Posts

Rais Samia Suluhu Hassan azungumza na Wananchi Liwale Mkoani Lindi

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Liwale katika Mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Viwanja vya Ujenzi Wilayani humo Mkoani Lindi ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya Maendeleo ya Wananchi katika Mikoa ya Kusini tarehe 17 Septemba, 2023. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akisalimiana na baadhi ya Watu wenye Ulemavu wakazi wa Liwale  mkoani Lindi mara baada ya kuhutubia Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Ujenzi Wilayani humo, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya Maendeleo ya Wananchi katika Mikoa ya Kusini tarehe 17 Septemba, 2023 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwapungia mkono Wananchi wa Wilaya ya Liwale mara baada ya kuwahutubia kwenye Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Ujenzi Wilayani humo, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya Maendeleo ya Wananchi...

TALGWU YATOA MAFUNZO KWA WAAJIRI HALMASHAURI ZA WILAYA MKOA WA SHINYANGA KUBORESHA MAZINGIRA YA WAAJIRI NA WAAJIRIWA

Image
  Mwenyekiti wa TALGWU na Rais wa Chama Cha Wafanyakazi Tanzania (TUCTA, Tumaini Nyamhokya, akifungu mafunzo hayo Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog   Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania (TALGWU) kimetoa mafunzo kwa Waajiri wa Halmashauri za Wilaya Mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya kuwajengea uwezo kuhusu masuala mbalimbali ya Vyama vya Wafanyakazi. Semina hiyo ya siku moja imefanyika leo Jumatano Septemba 20,2023 Mjini Shinyanga na kukutanisha pamoja viongozi wakuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania (TALGWU) na Waajiri wa Halmashauri za Wilaya (Wakurugenzi wa Halmashauri na Wakuu wa Rasilimali watu kutoka Halmashauri za wilaya Mkoani Shinyanga.   Akizungumza wakati akifungua Semina hiyo, Mgeni rasmi Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Mkoa wa Shinyanga, Manyama Katikiro  amesema mafunzo hayo yatasaidia kuongeza mahusiano mazuri baina ya TALGWU na waajiri ili kuboresha mazingira...

CP SUZAN KAGANDA ATOA TAARIFA YA MKUTANOJUMUIYA YA ASKARI WA KIKE DUNIANI IAWP AFRIKA CHAPTER NEW ZEALAND 2023.

Image
  Na Mwandishi wetu Jeshi la Polisi- Auckland New Zealand Kamishna wa Jeshi la Polisi wa kamisheni ya Utawala na Manejimenti ya Rasilimali watu CP Suzan Kaganda leo septemba 20, 2023 amewasilisha taarifa ya Mkutano wa Jumuiya ya Polisi wa kike ukanda wa Afrika IAWP Afrika chapter uliyofanyika mwishoni mwa mwezi Julai,za 2023 jijini Dar es salaam, katika Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya askari Polisi wa kike Duniani IWAP unaoendelea Auckland New Zealand. CP Suzan Kaganda amewasilisha taarifa hiyo katika Mkuu wa IWAP ambao umehudhuriwa na nchi (65) yakiwemo mataifa mengine ya Afrika ambayo ni Tanzania, Afrika kusini na Ghana ambapo kimefanyika kikao cha wanachama wa kudumu wa Jumuiya hiyo Annual General Meeting (AGM) ya IAWP, Tanzania ikiwa kanda ya 21 ya nchi ya SADC na mjumbe aliyechaguliwa kwa kanda hiyo ni kamanda wa Polisi Mkoa wa kipolisi Ilala kamishna msaidizi wa Polisi ACP Dr. Debora Magiligimba kutoka Tanzania. Aidha kamishna Kaganda ametumia fulsa hiyo kuwakaribis...

VIJANA WAFUNDISHWA UZALISHAJI BIDHAA,UFUGAJI NA UTAFUTAJI WA MASOKO

Image
   Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha Kilimo Kiuma kinachomilikiwa na kanisa la Upendo wa Kristo Masihi,wakimsikiliza Mkuu wa chuo hicho Fulko Hyera jana. Na Muhidin Amri ASILIMIA 85 ya wakazi wa mkoa wa Ruvuma na asilimia 75 ya Watanzania wanatajwa kutegemea sekta ya kilimo kuendesha maisha yao ya kila siku. Hata hivyo idadi hiyo itaongezeka baada ya serikali na wadau mbalimbali kuanza kuwekeza kwenye sekta hiyo  kwa kufungua mashamba makubwa na kuanzisha vyuo vya kilimo. Lengo la uwekezaji huo ni kuongeza uzalishaji wa mazao ili kujipatia kipato na  kuongeza idadi ya wataalam watakaotumia maarifa na elimu yao kufundisha kilimo cha kisasa na kwenda kuanzisha mashamba madogo na makubwa yatakayotumika kama mashamba darasa  kwa jamii yetu. Kanisa la Upendo wa Kristo Masihi-Kiuma lililopo katika kijiji cha Milonde kata ya Matemanga wilayani Tunduru limeanzisha chuo cha kilimo  na ufugaji ili kuwapatia  mafunzo ya kilimo cha ...