Posts

Airtel FURSA yawafungulia masoko mapya wajasiliamali wadogo wadogo jijini

Image
Mkuu wa wilaya ya Kindondoni Mh Aly Hapi akikagua na kujionea bidhaa za mjasiliamali aliyewezeshwa na Airtel FURSA Bi Betty Mngulwi mwisho mwa wiki ambapo Airtel iliwakutanisha baadhi ya wajasiliamali jijini Dar es salaam katika maonyesho maalum ya ‘Airtel FURSA Wajasiliamali Bazaar’ nje ya ofisi kuu ya Airtel Morocco kwa lengo la kuwakutanisha wajasiliamali hao na wateja mbalimbali ili kuwatanua masoko yao na kuuza bidhaa zao. pamoja nae ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Bi Beatrice Singano wakwanza kulia.   Mkuu wa wilaya ya Kindondoni Mh Ally Hapi akipokea zawadi ya keki toka kwa  mjasiliamali aliyewezeshwa na Airtel FURSA Bi Diana Moshi  mwishoni mwa wiki mara baada ya kutembelea banda la mjasiliamali huyo wakati wa  maonyesho ya  bidhaa za wajasiliamali katika maonyesho ya ‘Airtel FURSA Wajasiliamali Bazaar’ nje ya ofisi kuu ya Airtel Morocco yaliyoandaliwa na Airtel kwa lengo la kuwakutanisha wajasiliamali hao na wateja wa airtel il...

TLS,TWAWEZA: MUSWADA HUU WA SHERIA YA HUDUMA ZA HABARI MZURI

Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) na Taasisi ya Twaweza wamesema kuwa Muswaada wa Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 ni bora kuliko Miswada iliyowahi kuwasilishwa nchini. Haya yamebainishwa katika maoni yao waliyowasilisha kwenye Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii leo Mjini Dodoma katika juhudi za kuufanya Muswada huo kuwa bora zaidi na kupelekea kuapa sheria yenye tija kwa wananchi na taifa kwa ujumla. TLS na Twaweza wamebainisha kuwa Muswada huu ni bora zaidi   na utasaidia kuwajengea wadau wa habari nchini heshima kwa kutoa huduma bora kupitia   vyombo vya habari kwa kuzingatia taaluma ya Habari waliyonayo hatua ambayo inautofautisha na muswada uliowasilishwa Bungeni mwaka 2015. Kwa mujibu wa maoni yalitolewa na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) yamesema Muswada huo mzuri zaidi na unaifuta Sheria ya   Magazeti ya Mwaka 1976 hatua ambayo wameipongeza Serikali kwani Sheria hiyo   iliwahi kuainishwa kuwa miongoni mwa Sheria 40 ...

Golf katika Klabu jeshi la ulinzi la Wananchi wa Tanzania Lugalo

Image
Mcheza golf Mtoto Asnath Juma akiwa katika harakati za kupiga mpira katika mashindano yaliyohusisha vijana katika uwanja wa Klabu ya jeshi la Ulinzi la Wananchi ya Lugalo jijini Dar es Salaam (Picha na Luteni Selemani Semunyu). Mashindano ya mwisho wa Mwezi ya  Mchezo wa Golf katika Klabu jeshi la ulinzi la Wananchi wa Tanzani a  ya Lugalo yamefanyika huku Wachezaji wengi wakichezea viwango  vipya vya Uchezaji baada ya kufanya vizuri au vibaya katika mashindano ya Arusha Open na yale ya PWC yaliyofanyika Lugalo Jijini Dar Es Salaam. Katika Division A mshindi ni Juma L ikuli aliyepiga mikwaju ya jumla 76 huku kiwango chake cha uchezaji kikiwa ni 5 akifuatiwa na Saleh Mcharo  kwa count back  baada ys kupiga mikwaju ya jumla 77 huku kiwango cha uchezaji kikiwa ni Sita. Katika Division B Raji Lavingia aliyeshinda baada ya kufungana (count back) baada ya kupiga mikwaju ya jumla 69 huku kiwango chake cha Uchezaji kikiwa ni 14 akifuatiwa na Shaizad ...