Posts

Showing posts from April, 2025

HAKUNA MTANZANIA ATAKAYEKOSA HUDUMA ZA UGONJWA WA UKIMWI WAZIRI MKUU MAJALIWA

Image
WAZIRI  Mkuu , Kassim Majaliwa, amewataka   Watanzania kuendelea kuchukua tahadhari kwa kuwa ugonjwa wa UKIMWI bado ni tishio na  kiwango cha maambukizi mapya ni watu 60,000 kila mwaka ambapo vijana wanaopata VVU maambukizi ni takribani asilimia 34.3 ya maambukizi mapya.  Waziri Mkuu Majaliwa ameyasema hayo  Bungeni Jijini Dodoma wakati akisoma hotuba ya bajeti ya bajeti ya ofisi yake kwa mwaka wa fedha 2025/26 na kusema kuwa Serikali itaendelea kuratibu shughuli za UKIMWI kwa kutoa huduma endelevu na stahimilivu kwa WAVIU. “Serikali itaendelea kuimarisha Mfuko wa Udhamini wa UKIMWI ili uweze kufanikisha malengo ya nchi katika kutokomeza UKIMWI ifikapo 2030, kuweka msukumo katika kupunguza maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto,kuhamasisha mabadiliko ya tabia katika jamii ili kupunguza maambukizi mapya ya VVU,”amesema.  Sambamba na hayo, Serikali inatambua mabadiliko ya sera za misaada kutoka kwa baadhi ya wafadhili wa muda mr...

WAZIRI BASHE AWATOLEA UVUVI WAZUSHI WANAODAI CHAI YA TANZANIA KUKOSA UBORA KWENYE SOKO LA KIMATAIFA

Image
WAZIRI wa Kilimo, Hussen Bashe, amelaani madai kwamba chai ya Tanzania haiuziki Duniani, na kueleza wazi kuwa huo ni uzushi mkubwa na kusema watu hao walaaniwe. Akizungumza leo  kwenye mkutano mkuu wa wadau wa Tasnia ya Chai, Waziri Bashe amefichua kwamba uchunguzi wake umeonyesha kuna mahitaji makubwa ya chai ya Tanzania, lakini viwanda vyetu vinakabiliwa na changamoto za ubora. Waziri Bashe amesisitiza kuwa, umuhimu wa kuboresha mchakato wa uzalishaji ili bidhaa yetu iweze kushindana kimataifa. kulishika soko la hilo ni viwanda na wakulima kutimiza wajibu wao, wakulima walipwe haki zao na wazalishaji nao wazalishe bidhaa iliyo bora. "Tunahitaji kushirikiana kwa dhati kabisa kama wadau ili kuimarisha tasnia hii ya chai hapa nchini," Bashe alisema Kwa upande wa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, Deo Mwanyika,akizungumza katika Kongamano hilo alidai kilio kikubwa wanachokumbana nacho pindi wanapotembelea katika maeneo...