MRADI WA UMEME WA MAKAMBAKO HADI SONGEA UNAOFADHIRIWA NA NCHI YA SWEDEN WAFUNGWA MAHESABU YAKE.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati Mhandisi Felchesmi Mramba, akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumaliza mazungumzo na Balozi wa Swedeni nchini kuhusu kufunga mahesabu ya mradi wa umeme kutoka Makambako hadi Songea . mradi huo ulikuwa ukifadhiliwa na nchi hiyo, Katibu Mkuu aliipongeza nchi hiyo kwa kuweza kuinufaisha Tanzania kwa ufadhili wake. Katibu hyo alibainisha kwamba nchi hiyo imebakiza ufadhili wake katika maswala ya Umeme ni umeme wa Hale ambapo wanafanyia matengenezo makubwa , alibainisha kwamba umeme wa hale ulianza kutumika tangu mwaka 1964 sasa Sweden inakalabati ili uweze kutumika vyema kwa mikoa ya jirani na Tanga. Kushoto ni Balozi wa Sweden nchini Bii Charlotta Ozaki-Macias. Mradi huo ulianza kutekelezwa mwaka 2017 ulizinduliwa na Rais wa awamu ya tano hayati Dkt. John Joseph Magufuli, mradi huo ulifadhiliwa kwa mkopo na serikali ya swedeni na leo hii umefungwa rasmi, Mramba alibainishwa kwamba nchi hiyo imefadhili Tanzania kwa miradi ...