Posts

Showing posts from February, 2025

NAIBU WAZIRI WA KILIMO SILINDE AZINDUA MIRADI SAGCOT, AGRA JIJINI DODOMA

Image
Naibu Waziri wa Kilimo, David Silinde amezindua Miradi itakayosaidia kuleta zaidi mageuzi katika Sekta ya Kilimo, inayofahamika kama SAGCOT: Support to SAGGOT Centre Ltd; na AGRA: Support to Tanzania’s Agriculture Transformation Office. Dhumuni la miradi hiyo ni kupanua wigo wa maeneo ya Kilimo Tanzania, yaani “The Agriculture Growth Corridors of Tanzania (AGCOT) kufuatia kusainiwa kwa mkataba wa makubaliano kati ya Norway na AGRA.  Makubaliano hayo yamelenga kufungua vikwazo vya udhibiti wa kilimo ikiwa ni pamoja na vikwazo vya mauzo ya nje ili kuvutia uwekezaji wa Sekta Binafsi katika Sekta ya Kilimo nchini kupitia Ofisi ya Mageuzi ya Kilimo (Agricultural Transformation Office - ATO). Uzinduzi huo umefanyika tarehe 04 Februari 2025 jijini Dodoma na kuhudhuriwa pia na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Tine Tonnes; Mtendaji Mkuu wa Southern Agricultural Growth Corridor of Tanzania (SAGCOT), Bw. Geoffrey Kirenga; Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Ofis...

CCM KUFIKISHA MIAKA 48 YATUMIKA KUTAMBULISHA WAGOMBEA WAKE URAIS MWAKA HUU JIJINI DODOMA--CPA MAKALLA

Image
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), CPA .Amos Makalla, akizungumza na wanahabari leo jijini Dodoma , alisema kilele cha miaka 48 ya chama hicho tangu kuzaliwa kwake kitafanyika jijini Dodoma  tarehe 5.2.2025. na mgeni rasmi anatalajiwa kuwa mwenyekiti wa chama hicho Dkt. Samia Suluhu Hassan, Aidha Makalla, aliwaeleza wanahabri kuwa siku hiyo pia kitatumia maadhimisho hayo kuwatambulisha wagombea  wa nafasi za juu wa chama hicho Tanzania bara na Zanzibar. Makalla,amewaomba wanachama wa chama hicho na wapenzi wachama hiocho kujitokeza kwa wingi, amesema huo sio mkutano ni maadhimisho wanaalikwa wote mageti  ya Uwanaja wa Jamhuri yatakuwa wazi kuanzia saa 12 asubuhi. "Njooni kwenye jambo letu mshuhudie Chama imara chama Tawala kipenzi cha wananchi wa nchi hii na Dunia kwa ujumla, chama Dume kilichotumika kukomboa baadhi ya nchi za Bara la Afrika njoni mkishuhudie".  alisema Makalla. Wanahabari wakimsikiliza Katibu huyo  Mkuu wa Habari wa Idara...

PICHA ZA MATUKIO YA SIKU YA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SHERIA NCHINI

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwahutubia, Majaji, wageni waalikwa pamoja na wananchi kwa ujumla kwenye Maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini ambayo Kitaifa yamefanyika katika viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma tarehe 03 Februari, 2025. Rais Dkt, Samia Suluhu Hassan, spika wa Bunge Dkt. Tul;ia Ackson , J aji Mkuu wa Prof. Ibrahim Hamis Juma  na viongozi wengine wakiwa wamesimama  wakati wimbo wa Taifa ukipigwa na ule wa Afrika Mashariki  wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Sheria Nchini yaliyofanyika Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma leo February 03,2025 Jaji Mkuu wa Tanzania  Prof. Ibrahim Hamis Juma (katikati), akionoza maandamano ya Majaji kuingia katika eneo la maadhimisho ya siku ya sheria nchini  Wanakwanya wa Mahakama Kuu wakitoa burudani katika kilele hicho