Posts

Showing posts from January, 2025

MASHABIKI YANGA NA SIMBA KUONESHANA UBABE BUNGE BONANZA

Image
  Mashabiki wa Yanga wakiwa wamefunika kwa bendera mashabiki wa Simba wakati wa mkutano wa kutangaza Bonanza la mashabiki wa timu hizo kwenye ukumbi wa Bunge wa Msekwa Dodoma. Bonanza hilo  lililodhaminiwa na Benki ya Azania linafanyika  kwemye viwanja vya Shule ya John Merlin Miyuji, Dodoma. mashabiki wa Yanga wakionesha 5 watakazowafunga watani zao Simba wakiwa katika picha ya pamoja kuonesha umoja wa mashabiki hao wa Simba na Yanga.

MATUKIO YA PICHA ZA BUNGENI LEO

Image
Spika Dkt. Tulia Ackson, akisikiliza maoni ya wabunge leo asubuhi katika kipindi cha maswali na majibu Mbunge Askofu Gwajima akiuliza swali Mbunge Waitara, akiuliza swali Wageni  wa Spika kutoka Mbeya, wakipiga picha na baadhi ya wabunge wa mkoa huo  

MKUTANO WA 18 WA BUNGE UMEANZA LEO JIJINI DODOMA

Image
Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson, akiingia Bungeni kwa ajili ya kuanza vikao vya bunge leo jijini Dodoma Brasbendi ya Jeshi la Polisi ikipiga wimbo wa Taifa na wa Afrika Mashariki kuashiria kuanza kwa vikao vya bunge Naibu Waziri TAMISEMI, Zainabu Katimba, akitoka kujibu maswali ya wabunge  

RC MACHA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI MIKATABA 9 YA MIRADI YA MAJI KATI YA RUWASA NA WAKANDARASI

Image
Utiaji saini mikataba 9 ya ujenzi wa miradi ya maji kati ya Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) na wakandarasi likiendelea Na Marco Maduhu, SHINYANGA Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anamringi Macha, ameshuhudia utiaji saini mikataba 9 yenye thamani ya zaidi ya shilingi Bilioni 4.7 ya ujenzi wa miradi ya maji kati ya Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) na wakandarasi.  Hafla hiyo imefanyika leo, Januari 24, 2025, katika ukumbi wa mikutano wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga na ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na Chama. Akizungumza katika hafla hiyo, Macha ametoa pongezi kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha na kutekeleza miradi ya maji mkoani Shinyanga, akielezea kuwa juhudi hizo zitasaidia kutatua changamoto ya ukosefu wa maji kwa wananchi. Macha ameeleza kuwa mikataba hiyo ni ya ujenzi wa miradi ya maji yenye thamani ya shilingi bilioni 4.7, ambapo vijiji 16 vitapata huduma ya maji, na vituo 18 vya kuchotea maji vitajengwa.  Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anamr...