LOWASSA AKOMBA WAPIGA KURA KUSINI

 Mgombea wa Ubunge anaekubalika na wananchi wa Masasi kupitia Mwamvuli wa Chama cha Wananchi CUF, Ismail Makombe (Maarufu kwa Jina la Kundambada), akizungumza machache na wananchi hao waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Boma
 Mwenyekiti Mwena wa Ukawa, Dkt. Emmanuel Makaidi akiwa ameambatana na Mkewe, wakiwasalimia wananchi wa Mji wa Masasi, Mkoani Mtwara

Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akizungumza jambo na Mke wa Mwenyekiti wa Chama cha NLD, Dkt. Emmanuel Makaidi (kulia), Mama Modesta Makaidi, wakati wa Mkutano wa Kampeni,  uliofanyika kwenye Uwanja wa Boma

Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Edward Lowassa, akiwahutubia wananchi wa Mji wa Masasi, Mkoani Mtwara, waliofikia kusikiliza sera zake katika Mkutano wa hadhara wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Boma


 Lowassa, akiwa haamini umati wa watu waliokuja kumpokea na kuzungumza na kisha kuwaomba  kura kwake na kwa madiwani na wabunge wanaounda UKAWA
 Sehemu ya Umati wa Wananchi wa Mji wa Masasi, Mkoani Mtwara wakiwa wamefurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Boma, leowakimshangilia na kuuponda utafiti wa TWAWEZA
Akizungumza nao
 Lowassa kama Yohana mbatizaji  hana maneno mengi elimu, elimu elimu bulee mengine atayashughulikia kwa pamoja na wananchi wenyewe
Akiondoka na kuwaaga katika eneo hilo.


Wajibuni Twaweza kwa kura-Lowassa
Tuwajibu Twaweza kwa mafuriko ya kura- Lowassa
MUDA  mfupi baada ya Twaweza kutoa matokeo ya utafiti yaliyoonyesha mgombea uraisi wa CCM , Dk John Mafufuli anaongoza, Waziri Mku wa Zamani, Edward  Lowassa, anayepeperusha bendra ya Chadema, aliwataka wananchi kujibu utafi huo kwa kura.
Mgombea huyo anayeungwa mkono na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), alisema yeye anasubiri mafuriko ya kura Okatoba 25.
 Akizungumza jana kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika Viwanja vya Madeko kwenye Jimbo la Ndanda wilayani Masasi katika Mkoa wa Mtwara, Lowassa alisema “leo asubuhi (jana) kuna watu  waliotoa matokeo ya kura ya maoni wakasema eti Magufuli amepata kama asilimiwa 65 mimi 25”
Wananachi “ waongoo”
“Sisi tujipange tuwajibu kwenye kura. Nangonja kwa hamu mafuriko ya kura, kutoka kwa wana ndanda Watanzania wote.
Tarehe 25 mnipe kura, mtashindwa kuona hizi mvi?,” alisema Lowassa huku akiwa navua kofia.
Naye Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye  akizungumzia suala hilo, alisema utafiti huo umepikwa ili kuwahadaa wananchi wajue kwamba Dk magufuli ndiye anayependwa zaidi na wananchi.
“Leo wametoa utafiti feki, hewa, uliotengenezwa. Wanasema ati leo kura ikipigwa Magufuli atapata kura asilimia  65,  na Lowassa asilimia 25,” alisema Sumaye huku baadhi ya wananchi wakijibu “Waongoo.”
Sumaye aliendelea kusema kuwa, “tumepita mikoa kibao watu kwa maelfu wanakuja na kutaka mabadilik;o, wao wakija hapa watu hawafiki hata robo ya ninyia, Dk Magufuli mpaka azoe watu na malori.”
Alisema hakuna jema lolote mpaka sasa ambalo CCM imefanya, “ leo wanataka kucheza na akili za watu ili watu wajue kuwa Magufuli ndiye anayependwa.”
Nataka maendeleo
Akizungumzia suala la Maendeleo, Lowassa alisema amechoka na umasikini ambao umekuwa ikiimbwa tangu mwaka 1962.
Alisema atataka wananchi wawe huru ndani ya nchi yao ili kama ni wakitaka kuuza mazao ya ya biashara wafanye hivyo sehemu yoyote.
“Na nitaanza na eneo la elimu, kubadili mfumo wa elimu na maslahi ya elimu yawe bora na kilimo cha kisasa. Nilivyokuwa Bukoba nilisema kama Kahawa Uganda ni bei nzuri watu waruhusiwe kuuza huko.
Lazima raia wawe huru, kama ulikuwa uwasaidii wananchi wakati wakati wanalima kwanini uwaingilie wakati wa kuuza?,” alisema Lowassa.
Kuhusu suala la gesi asili, alisema serikali ya Ukawa ikiingia madarakani ahatahakikisha wanapitia upya mikataba ya gesi na mafuta ili kuona kama inanufaisha wananchi, haswa wale wa mikoa ya kusini na Watanzania kwa ujumla.
Sumaye: Ule wako Nape
Sumaye alisema baada ya kuzungumza mambo mbalimbali ya serikali ameanza kutishwa ikiwa ni pamoja na Kauli ya Katibu Mwenezi wa CCM, Nape Nnauye aliyemtaka kiongozi huyo kunyamaza vinginevyo atamshughulikia.
“Anasema Sumaye anyamaze vinginevyo tutamshukunghulikia, sijui atanishughulikia kwa lipi, lakini ole wake nikipata tatizo lolote.
Nataka wapande jukwaani watuambie madawa ya kulenya yanayokamatwa kila siku kwa maguni ni ya nani na mpaka sasa kafanywa nini?
Meno ya tembo ya tembo yanayokamatwa huko ni ya nani na mpaka sasa hivi kafanywa nini?
Meli mbovu iliyopo Dar es Salaam ambayo sasa imeletwa Lindi ili kuwadanganywa wananchi nani kainunua na kafanywa nini, mabehewa mabovu nani kanunua na kachukulia hatua gani.
Siyo nikisema haya unasema utanishughulikia, utanishughulikia we nani?
Kama hawana majibu ya haya lazima waondoke, ndiyo utaratibu duniani kote, wanashangaa nini?
Kama hawataki kuondoka wasema kuwa wao ni madkteta tujue.
Kama ni chama cha siasa kama vingine, Oktoba 25 wanaondoka asubuhi,” alisema Sumaye.
 Sumaye alisema hali ya kutishwa haipo kwake pekee bali hata kwa wananchi ambao wanadanganywa kuwa wakichagua upinzani nchi itakuwa na vita.
Alisema Libya, Misri ilipata machafuko baada ya serikali kukataa kusikiliza wananchi.
“Ndiyo hivyo CCM wanataka kufanya, wakikataa itakuja kutokea hayo, watakaoamua kiti cha urais kiende wapi ni kura zenu,” alisema Sumaye.
Nguvu ya Umma na wabunge
Lowassa jana alilazimika kutumia mahakama ya wananchi kuchagua Mgombea Ubunge wa Jimbo la Masasi ambapo kulikuwa na msuguano wa Chadema na NLD.
Katika jimbo hilo, Chadema wamemsimamisha Cecil David Mwambe, huku NLD ikimsimamisha Angelous Gadriel Thomas.
Kutokana na hali hiyo, wagombea wote hao walipewa nafasi ya kupanda jukwaani na kila mmoja kwa wakati wake aelekeze changamoto za jimbo la Ndanda.
Baada ya kunadi sera zao, Lowassa kabla ya kumaliza kuhutubia aliwaita wagombea hao na kisha kihoji wananchi ni nani wanayemtaka na uwanja mzima ukamchagua Mwambe.
Lowassa alihoji wananchi hao mara mbili kisha kumuuliza mgombea na NLD kama anakubaliana na matokeo.
“Sikubaliani nayo kwa sababu yalishapangwa,” alisema.
Baada ya kauli hiyo Lowassa alisema kwa mamlaka aliyopewa anamtangaza mgombea wa Chadema kuwa mgombea wa jimbo hilo kwa kuwa amekubaliwa na wananchi walio wengi.


Comments