WAGONJWA 19,371 WATIBIWA KATIKA TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE KUTOKA JANUARI HADI MACHI 2018.



Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kipindi cha miezi mitatu ya Januari hadi Machi 2018 imeona jumla ya wagonjwa 19,371 wenye matatizo mbalimbali ya moyo kati ya hao wagonjwa wa nje ni 18,481 na waliolazwa ni 890.

Wagonjwa 105 walifanyiwa upasuaji wa moyo wa kufungua kifua kati ya hao watu wazima 53 na watoto 52. Kati ya wagonjwa 105 waliofanyiwa upasuaji 66 walifanyiwa na madaktari wetu bingwa wa magonjwa ya moyo watoto wakiwa ni 35 na watu wazima 31.

Upasuaji wa moyo wa bila kufungua kifua (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab ulifanyika kwa wagonjwa 231 kati ya hao watoto ni 20 na wakubwa 211. Kati ya wagonjwa 231 waliotibiwa wagonjwa watu wazima 211 walifanyiwa upasuaji na madaktari wetu wa ndani.
Kwa kipindi cha miezi mitatu tumekuwa na jumla ya kambi za matibabu nane (8) ambapo tulifanya matibabu kwa kushirikiana na washirika wetu kutoka nchi za Ujerumani, Israel, Australia , Marekani, India na Falme za Kiarabu. Katika kambi hizo jumla ya wagonjwa 39 walifanyiwa upasuaji wa kufungua kifua kati ya hao watoto 17 na watu wazima 22. Wagonjwa 72 walifanyiwa upasuaji wa bila kufungua kifua kati ya hao watoto 20 na watu wazima 52.
Tumefanya upasuaji wa kuunganisha mishipa ya damu (AVF- Arterio Venous Fistula) kwa ajili ya kusafishia damu kwa wagonjwa wenye matatizo ya figo (Hemodialysis) 36.
Changamoto kubwa tunayokabiliana nayo ni wagonjwa wengi tunaowapokea mioyo yao kutokuwa katika hali nzuri hivyo basi tunawaomba wananchi kujenga tabia ya kupima afya zao mara kwa mara hii itawasaidia kujuwa kama wana matatizo ya moyo au la na kama wanamatatizo wataweza kupata tiba kwa wakati.
Wazazi na walezi tunawaomba wasisahau kupima afya za watoto wao pale watakapoona kuna hali ya tofauti katika ukuaji wa mtoto kwani magonjwa mengi ya moyo yanaanzia utotoni. Mtoto akianza kuuguwa magonjwa ya moyo wazazi wengi wanadhani ni matatizo ya kifua baada ya kumfikisha Hospitali na kufanyiwa vipimo ndipo inagundulika mtoto anasumbuliwa na magonjwa ya moyo. Kwa wamama wajawazito wafanye uchunguzi (Fetal Echocardiography) wa kuangalia kama mtoto aliyeko tumboni anamatatizo ya moyo.
Aidha kwa upande wa gharama za matibabu Taasisi yetu imeyagawa katika makundi manne (4) tuna wagonjwa wanaotibiwa kwa bima mbalimbali ambazo tumeingia makataba nazo. Wagonjwa wanaolipia gharama zote wenyewe, wagonjwa wanaochangia kidogo huku gharama zingine zikilipwa na Serikali. Kundi la mwisho ni wagonjwa ambao hawalipii kabisa gharama za matibabu ikiwa watakidhi vigezo vyote vya kutokulipa.
Huduma zetu za matibabu ya moyo zinatolewa kwa watanzania wote wa Bara na Visiwani. Ifahamike kwamba fedha za matibabu zinazolipwa na wagonjwa zinatumika kununua vifaa tiba vya moyo kama mlango wa moyo (Valve), betri ya moyo (Pacemaker) na vinginevyo.
Kutokana na matibabu ya moyo kuwa ya gharama kubwa tunaendelea kuwasisitiza wananchi wajiunge na mifuko ya bima za afya ambayo itawasaidia kulipa gharama za matibabu pindi watakapohitaji kutibiwa. Pia itasaidia Hospitali yetu kuendelea kujiendesha yenyewe kwa kushirikiana na Serikali na wadau wengine.

Imetolewa na:
Kitengo cha Uhusiano
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
19/04/2018

UJANGILI NCHINI WAPUNGUA KWA ZAIDI YA ASILIMIA 50 - DK. KIGWANGALLA


Na Hamza Temba-Dodoma
Serikali imefanikiwa kudhibiti vitendo vya ujangili hapa nchini kwa zaidi ya asilimia 50.

Hayo yameelezwa jana na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla wakati akizungumza na Balozi wa Uingereza hapa nchini, Sarah Cooke ofisini kwake mjini Dodoma.

Mazungumzo hayo yalilenga kujadili mambo mbalimbali ikiwemo kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo mbili katika sekta ya uhifadhi na maendeleo ya utalii.Dk. Kigwangalla alisema katika kipindi cha miezi sita iliyopita hakuna mauaji mapya ya wanyamapori yaliyoripotiwa na kwamba nyara zinazokamatwa hivi sasa ikiwemo meno ya tembo na ngozi za wanyamapori ni masalia ya zamani.

Amesema mafanikio hayo yametokana na juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali kudhibiti vitendo vya ujangili ikiwemo doria za mara kwa mara za kiitelijensia ambazo zimekuwa zikishirikisha vyombo mbalimbali vya ulinzi na usalama pamoja na raia wema. 

Alisema Serikali itaendelea kudhibiti vitendo hivyo kwa kuimarisha ulinzi katika maeneo ya hifadhi nchini ikiwa ni pamoja na kuanzisha jeshi maalum la usimamizi wa Misitu na Wanyamapori, Sheria ya wanyamapori na za taasisi za uhifadhi zimeanza kufanyiwa marekebisho kuwezesha mabadiliko hayo.

Katika hatua nyingine Dk. Kigwangalla amemueleza balozi Cooke kuwa, Serikali kupitia Wizara yake inaendelea kuimarisha  vivutio vya utalii hapa nchini kwa kupanua jeografia ya maeneo ya utalii sambamba na kuongeza vivutio ili kuongeza idadi ya watalii na mapato.

Amesema Serikali itajenga makumbusho ya Marais Wastaafu wa Tanzania mjini Dodoma pamoja kuanzisha makumbusho ya meno ya tembo katika miji ya Dar es Salaam, Arusha, Iringa na Dodoma.

Sambamba na hayo amesema Serikali itaanzisha mwezi maalum wa maadhimisho ya urithi wa Mtanzania ambao utafanyika mwezi Septemba kila mwaka pamoja na kuendeleza utalii wa mikutano.

Amesema Serikali pia itaanzisha Mamlaka ya Usimamizi na Uendelezaji wa Fukwe nchini ili kuimarisha utalii wa fukwe pamoja na kutambua barabara iliyokuwa ikitumika katika biashara ya utumwa wakati wa ukoloni ili iweze kutumika kiutalii.

Akizungumzia migogoro ya mipaka iliyopo baina ya wananchi na maeneo ya hifadhi, Dk. Kigwangalla alisema Serikali itatatua migogoro hiyo kwa kushirikisha wananchi sambamba na kuwasaidia kutatua changamoto za msingi ambazo ni kuimarisha maeneo ya malisho ya mifugo, upatikanaji wa maji kwa ajili ya wananchi na mifugo, mpango bora wa matumizi ya ardhi na uendelezaji wa kilimo na ufugaji.

Kwa upande wake balozi Cooke alisema nchi yake itaendelea kuimarisha ushirikiano inaoutoa kwa Serikali ya Tanzania katika kudhibiti mtandao wa uhalifu wa madawa ya kulevya, rushwa na ujangili.

Alisema kwa sasa watalii zaidi ya 75,000 wa Uingereza hutembelea Tanzania kila mwaka na wengine wamewekeza katika sekta utalii hapa nchini, hivyo akaiomba Serikali kurekebisha baadhi ya changamoto chache zilizopo katika sekta hiyo kwenye mtiririko wa kodi. 


Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na balozi wa Uingereza hapa nchini, Sarah Cooke ofisini kwake mjini Dodoma jana ambapo walijadili mambo mbalimbali ya kuimarisha ushirikiano katika sekta ya uhifadhi na maendeleo ya utalii.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na balozi wa Uingereza hapa nchini, Sarah Cooke ofisini kwake mjini Dodoma jana ambapo walijadili mambo mbalimbali ya kuimarisha ushirikiano katika sekta ya uhifadhi na maendeleo ya utalii.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla.
 Balozi wa Uingereza hapa nchini, Sarah Cooke.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiaga na balozi wa Uingereza hapa nchini, Sarah Cooke ofisini kwake mjini Dodoma jana baada ya mazungumzo yaliyolenga walijadili mambo mbalimbali ya kuimarisha ushirikiano katika sekta ya uhifadhi na maendeleo ya utalii.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiagana na msafara wa balozi wa Uingereza hapa nchini, Sarah Cooke ofisini kwake mjini Dodoma jana ambapo walijadili mambo mbalimbali ya kuimarisha ushirikiano katika sekta ya uhifadhi na maendeleo ya utali 

Wednesday, April 18, 2018

Wadau wa dawa na vifaa tiba nchini watakiwa kuchangamkia fursa

Nteghenjwa Hosseah, OR-TAMISEMI.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Mhe. Josephat Kandege amewataka wauzaji, waagizaji, wasambazaji na wadau wote wa dawa pamoja na Vifaa Tiba Nchini kuchangamkia fursa inayotolewa na Serikali ya kuwa Mshitiri mteule ‘Prime Vendor’ kusaidia katika utoaji wa dawa katika Mikoa yote Tanzania.

Kandege ameyasema hayo wakati akifungua kikao cha Wadau wa dawa  ‘Vendors Forum’ kilichoandaliwa na Ofisi ya Rais Tamisemi kwa kushirikiana na wadau wa Afya ‘HPSS’ chenye lengo la kuweka uelewa wa pamoja kuhusu uanzishwaji na utekelezaji wa mfumo wa Mshitiri.

Amesema “mfumo huu utatumika kupata mahitaji ya bidhaa za Afya pale ambapo vituo vya kutolea huduma za Afya vya Umma vitakosa au kupata kiwango pungufu toka Bohari Kuu ya Dawa na pia utasaidia kupunguza kero za Afya ikiwemo uhaba wa upatikanaji wa dawa kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya”.

Sasa basi ninyi kama wazabuni muhimu katika sekta hii ya Afya wenye Uzalendo na nia njema na Nchi ya Tanzania mnatakiwa kujitokeza katika mchakato wa kumpata Mshitiri (Prime Vendor) wa kila Mkoa ambaye atakidhi vigezo kwa mujibu wa taratibu manunuzi alisema Mhe. Kandege.

Wakati huo huo Naibu Waziri Kandege aliwafahamisha wadau wa dawa kuwa Serikali imagatua mipango na bajeti kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya na inapeleka Fedha moja kwa moja kwenye akaunti za benki zilizofunguliwa katika kila kituo hii itasaidia katika kufanya manunuzi ya dawa hizo na kurahisha mchakato wa malipo.

“Hivyo niwahakikishie kuwa utaratibu wa malipo utakua ni rahisi na wa haraka zaidi kwa kuwa Hospital, Vituo vya Afya na Zahanati husika zitahusika kuagiza dawa kwa Mshitiri pale mahitaji ya dawa hizo zitakapokosekana kutoka MSD” alisema Mhe. Kandege.

Alimalizia kwa kuwataka Wadau wote wa Dawa kutumia kikao hiki kuelewa kwa undani kuhusu utaratibu huu na kujitokeza kwa wingi katika mchakato wa kumpata Mshitiri Mteule kwani zoezi hili litaendeshwa kwa uwazi na kwa usindani mkubwa.

Mkurugenzi wa Afya Ofisi ya Rais Tamisemi Dr. Ntuli Kapologwe amesema hivi sasa wako katika uwekezaji Mkubwa katika Sekta ya Afya kwa kuzingatia kuwa Bajeti ya Dawa imeongezwa kutoka Bil 31 kwa mwaka 2015/16 hadi kufikia Bil 269 kwa mwaka 2017/18 hivyo ongezeko hili la bajeti linatakiwa kwenda sambamba na uhakika wa upatikanaji wa dawa na zenye ubora chini ya usimamizi makini wa wataalamu wa Afya.

Dr. Ntuli alisema mpango huu utaleta manufaa kwa wananchi wote ambao watakua chini ya mpango wa Tele kwa Tele na wale wanaopata huduma kupitia mfuko wa Bima ya Afya iliyoboreshwa; Tunataka kila mmoja apate dawa anayoihitaji kwa wakati.

Naye Mfamasia toka Ofisi ya Rais Tamisemi Regina Richard alisema mfumo wa Mshitiri Mteule umeanzishwa kwa sababu ya changamoto zilizoonekana awali za kutumia mzabuni kama vile taratibu za manunuzi kuchukua muda mrefu na gharama za manunuzi kuwa kubwa na zinazotofautiana kati ya Halmashauri moja na nyingine ndani ya Mkoa mmoja.

Changamoto zingine alizozibainisha ni kubadilika kwa bei mara kwa mara kila manunuzi yanapofanyika, kutokuwa na uhakika wa ubora wa bidhaa kutokana na kuhifadhiwa na kusafirishwa katika mazingira mbayo si salama na zaidi baadhi ya wazabuni na watumishi kutokuwa waaminifu.

Matumizi ya mfumo huu umeelekezwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi, Sera ya Afya ya Taifa ya mwaka 2007, Mpango Mkakati wa Sekta ya Afya na Sera ya Mashirikiano kati ya Serikali na Sekta binafsi.
Kikao hiki cha wadau wa dawa ‘Vendor Forum’ kimefanyika kwa mara ya kwanza na kimehusisha wadau kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara.
 Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Josephat Kandege(mbele) akifungua kikao cha wadau wa Afya ‘Vendor Forum’ kilichofanyika katika Ukumbi wa Dodoma Hotel.
  Mkurugenzi wa Afya Ofisi ya Rais Tamisemi Dr. Ntuli Kapologwe akitoa maelezo ya awali kabla hajamkaribisha mgeni rasmi kufungua kikao cha wadau wa Afya Vendor Forum.
 Mfamasia Mwandamizi  toka Ofisi ya Rais Tamisemi Regina Richard akielezea malengo la kikao cha Wadau wa Dawa ‘Vendor Forum’ kilichofanyika katika ukumbi wa Dodoma Hotel mapema leo.
  Wataalam toka Idara ya Afya Ofisi ya Rais-TAMISEMI pamoja na wadau wa Dawa wakiwa katika kikao maalum cha wadau wa dawa.


Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Josephat Kandege(mbele katikati) katika picha ya pamoja na baadhi ya wataalamu na wadau wa dawa.

Wadau wa dawa na vifaa tiba nchini watakiwa kuchangamkia fursa

Nteghenjwa Hosseah, OR-TAMISEMI.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Mhe. Josephat Kandege amewataka wauzaji, waagizaji, wasambazaji na wadau wote wa dawa pamoja na Vifaa Tiba Nchini kuchangamkia fursa inayotolewa na Serikali ya kuwa Mshitiri mteule ‘Prime Vendor’ kusaidia katika utoaji wa dawa katika Mikoa yote Tanzania.

Kandege ameyasema hayo wakati akifungua kikao cha Wadau wa dawa  ‘Vendors Forum’ kilichoandaliwa na Ofisi ya Rais Tamisemi kwa kushirikiana na wadau wa Afya ‘HPSS’ chenye lengo la kuweka uelewa wa pamoja kuhusu uanzishwaji na utekelezaji wa mfumo wa Mshitiri.

Amesema “mfumo huu utatumika kupata mahitaji ya bidhaa za Afya pale ambapo vituo vya kutolea huduma za Afya vya Umma vitakosa au kupata kiwango pungufu toka Bohari Kuu ya Dawa na pia utasaidia kupunguza kero za Afya ikiwemo uhaba wa upatikanaji wa dawa kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya”.

Sasa basi ninyi kama wazabuni muhimu katika sekta hii ya Afya wenye Uzalendo na nia njema na Nchi ya Tanzania mnatakiwa kujitokeza katika mchakato wa kumpata Mshitiri (Prime Vendor) wa kila Mkoa ambaye atakidhi vigezo kwa mujibu wa taratibu manunuzi alisema Mhe. Kandege.

Wakati huo huo Naibu Waziri Kandege aliwafahamisha wadau wa dawa kuwa Serikali imagatua mipango na bajeti kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya na inapeleka Fedha moja kwa moja kwenye akaunti za benki zilizofunguliwa katika kila kituo hii itasaidia katika kufanya manunuzi ya dawa hizo na kurahisha mchakato wa malipo.

“Hivyo niwahakikishie kuwa utaratibu wa malipo utakua ni rahisi na wa haraka zaidi kwa kuwa Hospital, Vituo vya Afya na Zahanati husika zitahusika kuagiza dawa kwa Mshitiri pale mahitaji ya dawa hizo zitakapokosekana kutoka MSD” alisema Mhe. Kandege.

Alimalizia kwa kuwataka Wadau wote wa Dawa kutumia kikao hiki kuelewa kwa undani kuhusu utaratibu huu na kujitokeza kwa wingi katika mchakato wa kumpata Mshitiri Mteule kwani zoezi hili litaendeshwa kwa uwazi na kwa usindani mkubwa.

Mkurugenzi wa Afya Ofisi ya Rais Tamisemi Dr. Ntuli Kapologwe amesema hivi sasa wako katika uwekezaji Mkubwa katika Sekta ya Afya kwa kuzingatia kuwa Bajeti ya Dawa imeongezwa kutoka Bil 31 kwa mwaka 2015/16 hadi kufikia Bil 269 kwa mwaka 2017/18 hivyo ongezeko hili la bajeti linatakiwa kwenda sambamba na uhakika wa upatikanaji wa dawa na zenye ubora chini ya usimamizi makini wa wataalamu wa Afya.

Dr. Ntuli alisema mpango huu utaleta manufaa kwa wananchi wote ambao watakua chini ya mpango wa Tele kwa Tele na wale wanaopata huduma kupitia mfuko wa Bima ya Afya iliyoboreshwa; Tunataka kila mmoja apate dawa anayoihitaji kwa wakati.

Naye Mfamasia toka Ofisi ya Rais Tamisemi Regina Richard alisema mfumo wa Mshitiri Mteule umeanzishwa kwa sababu ya changamoto zilizoonekana awali za kutumia mzabuni kama vile taratibu za manunuzi kuchukua muda mrefu na gharama za manunuzi kuwa kubwa na zinazotofautiana kati ya Halmashauri moja na nyingine ndani ya Mkoa mmoja.

Changamoto zingine alizozibainisha ni kubadilika kwa bei mara kwa mara kila manunuzi yanapofanyika, kutokuwa na uhakika wa ubora wa bidhaa kutokana na kuhifadhiwa na kusafirishwa katika mazingira mbayo si salama na zaidi baadhi ya wazabuni na watumishi kutokuwa waaminifu.

Matumizi ya mfumo huu umeelekezwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi, Sera ya Afya ya Taifa ya mwaka 2007, Mpango Mkakati wa Sekta ya Afya na Sera ya Mashirikiano kati ya Serikali na Sekta binafsi.
Kikao hiki cha wadau wa dawa ‘Vendor Forum’ kimefanyika kwa mara ya kwanza na kimehusisha wadau kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara.
 Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Josephat Kandege(mbele) akifungua kikao cha wadau wa Afya ‘Vendor Forum’ kilichofanyika katika Ukumbi wa Dodoma Hotel.
  Mkurugenzi wa Afya Ofisi ya Rais Tamisemi Dr. Ntuli Kapologwe akitoa maelezo ya awali kabla hajamkaribisha mgeni rasmi kufungua kikao cha wadau wa Afya Vendor Forum.
 Mfamasia Mwandamizi  toka Ofisi ya Rais Tamisemi Regina Richard akielezea malengo la kikao cha Wadau wa Dawa ‘Vendor Forum’ kilichofanyika katika ukumbi wa Dodoma Hotel mapema leo.
  Wataalam toka Idara ya Afya Ofisi ya Rais-TAMISEMI pamoja na wadau wa Dawa wakiwa katika kikao maalum cha wadau wa dawa.


Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Josephat Kandege(mbele katikati) katika picha ya pamoja na baadhi ya wataalamu na wadau wa dawa.

CCM DAR YASHAURI WALIOZIBA NJIA ZA MAJI WAONDOLEWE, YATOA POLE KWA WALIOPOTEZA NDUGU KWASABABU YA MVUA

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

CHAMA Cha Mapinduzi(CCM), Mkoa wa Dar es Salaam kimetoa pole kwa familia ambazo zimepoteza ndugu zao kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha huku kikitoa ushauri kwa Serikali kuwaondoa waliojenga kwenye njia za maji kwa lengo la kupunguza maafa.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam Cylivia Katekamba amewaambia leo waandishi wa habari kuwa chama hicho kinatoa pole kwa wote ambao wamefikwa na maafa na kuomba wenye uwezo wa kusaidia walioathrika na mvua hizo kujitokeza kusaidia.
" Mkoa wa Dar es Salaam umekumbwa na mafuriko na kusababisha baadhi ya wananchi kupoteza maisha.CCM mkoa tunatoa pole kwa ndugu, jamaa na marafiki kutokana na kuondokewa na ndugu zetu kutokana na mvua.
"Tunafahamu matatizo ya mafuriko yametokea kwetu na hata maeneo mengine duniani nayo wakati mwingine hukumbwa na mafuriko.Kubwa ni kuendelea kushikamana na kusaidia kwenye kipindi hiki.CCM tunatoa pole,"amesema Katekamba.
Pia ametoa mwito kwa walio maeneo hatarishi ni vema wakaondoka maeneo hayo na kufafanua kutokana kuzibwa kwa mitaro na njia za maji imesababisha hata maeneo ambayo huwa hayapati mafuriko safari hii maji yamejaa.
Amefafanua yapo maeneo ambayo watu wamejenga lakini kiuhalisia ni maeneo ambayo yapo kwa ajili ya kupitisha maji na matokeo yake yanakosa pakupita na kwenda kwenye makazi ya watu na kusababisha maafa.
Ameshauri watu wa mipango miji kuangalia namna ya kuondoa changamoto hiyo na kuongeza kamati ya siasa ya Mkoa wa Dar es Salaam jana usiku imekutana kujadili hali ya mafuriko."Moja ya jambo tulilokubaliana maeneo ambayo yanatakiwa kubaki wazi ili maji yapite lazima mipango miji kuangalia namna ya kufanya,"amesema na kuongeza ni vema wananchi wa wakazingatia utunzaji wa mazingira kwa kutoziba njia za maji na kutokata miti ovyo.
Alipoulizwa kuhusu waliojenga kwenye njia za maji, Katekamba amejibu kuwa kazi ya Chama ni kuisimamia Serikali na hivyo moja ya jambo ambalo wanataka kuona linafanyika ni kuwaondoa waliojenga maeneo hayo.
Pia ameomba wananchi kuibua na kuwabainisha watu ambao wamejenga kwenye mifereji ya kupitisha maji badala ya kukaa kimya huku akielezea CCM Mkoa wa Dar es Salaam walikuwa na sherehe yao ya familia ya Wana-CCM Aprili 21 mwaka huu ambayo Mwenyekiti wake ni Idd Azan lakini wameiahirisha kutokana na mafuriko ya mvua na athari zilizotokea. 
Hata hivyo, Katekamba pamoja na viongozi wengine wa ngazi mbalimbali ya mkoa wamefanya ziara ya kukagua mitaa iliyokumbwa na mafuriko na kuona hali halisi.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Mkoa wa Dar es Salaam Cylivia Katekamba(wa kwanza kushoto) akizungumza ma waandishi wa habari leo jijini wakati anatoa pole kwa waliokumbwa na mafuriko na familia ambazo zimepoteza wapendwa wao kwasababu ya mvua zinazonyesha.

Watanzania wahimizwa kujenga utamadunI wa kujisomea vitabu

Watanzania wamehimizwa kujenga utamaduni wa kujisomea vitabu kwa ajiri ya kuibua fursa mbalimbali za kimaendeleo na kuacha tabia ya  kutumia vitabu kama sehemu salama ya kuhifadhia fedha ,  kama ilivyo kwa baadhi ya watu maeneo ya vijijin na mjini  huku waandishi wa vitabu wakitakiwa kuendelea kuandika vitabu kwa lengo la kujenga Taifa lenye wasomi.


Hayo yamesemwa na mkuu wa chuo kikuu cha Mzumbe Prof, Ganka Nyamusogoro wakati wa uzinduzi wa siku ya kusoma vitabu duniani katika chuo kikuu cha Mzumbe mkoani Morogoro, ambapo amesema  jamii nyingi za kitanzania zimejenga tabia ya kutosoma vitabu kama njia ya kuibua fursa  na kuongeza maarifa baadala yake wanatumia  vitabu kama sehemu ya kuhifadhia fedha  jambo ambalo ni kinyume na na malengo ya waandishi wa vitabu.
 Makamu mkuu wa chuo kikuu cha Mzumbe  Prof,Ganka Nyamusogoro akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa siku ya kusoma vitabu Duniani katika chuo kikuu cha Mzumbe mkoani Morogoro.
 Makamu mkuu wa chuo kikuu cha Mzumbe  prof,Ganka Nyamusogoro akikagua moja ya vitabu vilivyooneshwa na chuo cha mzumbe wakati wa maadhimisho ya siku ya kusoma vitabu Duniani,ambapo chuo cha mzumbe kimetoa nafasi kwa watu mbalimbali kusoma vitabu katika eneo hilo ambalo lipo maalumu kwa siku tatu chuoni hapo kuadhimisha siku hiyo ya kusoma vitabu.
 Wanafunzi wa chuo kikuu cha mzumbe  mkoani Morogoro na shule ya sekondari Mzumbe wakifuatilia kwa umakini hotuba ya mgeni rasmi  katika maadhimisho ya siku ya kusoma vitabu duniani ambaye pia ni makamu mkuu wa chuo hicho Prof, Ganka Nyamusongoro hayupo pichani.
 Diwani wa kata ya Mzumbe mkoani Morogoro Recho Kungi wa kwanza kushoto  akisisitizia wanafunzi  juu ya umuhimu wa kusoma vitabu katika maadhimisho ya siku ya kusoma vitabu duniani yaliyo fanyika chuo kikuu cha Mzumbe mkoani Morogoro.
  Makamu mkuu wa chuo kikuu cha Mzumbe  Prof,Ganka Nyamusogoro ambaye pia ni Mgeni rasimi katika maadhimisho ya siku ya kusoma vitabu duniani chuo kikuu Mzumbe  Mkoani Morogoro  akisoma vitabu vya tafiti vilivyofanywa na wanazuoni wa chuo kikuu cha mzumbe mara baada ya kuzindua hafla hiyo.
 Mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari Mzumbe mkoani Morogoro Alfred  Joseph King akijisomea jarida wakati wa maadhimisho ya siku ya kusoma vitabu  duniani, jarida hilo  limechapishwa na chuo kikuu cha Mzumbe mkoani Morogoro.
 Makamu mkuu wa chuo kikuu cha Mzumbe  Prof,Ganka Nyamusogoro (katikati) akiangalia hotuba inayohusu maadhimisho ya siku ya vitabu  duniani ambapo kushoto kwake ni mkuu wa idara ya huduma za wasomaji chuo kikuu cha mzumbe Sarah Mwambalaswa na kulia ni Mkurugenzi maktaba na huduma za kiufundi chuo kikuu mzumbe Dk Arobogasti Musabila .
Wa kwanza kushoto ni David Onyango mkutubi wa maktaba ya chuo kikuu cha mzumbe akimuonesha vitabu vilivyo pangwa katika maktaba maalumu ya madhimisho ya siku ya kusoma vitabu duniani,wa pili kushoto Makamu mkuu wa chuo kikuu cha Mzumbe  Prof,Ganka Nyamusogoro anae fatia ni Diwani wa kata ya Mzumbe mkaoni Morogoro Recho Kungi wa mwisho ni  mkurugenzi maktaba na huduma za kiufundi chuo kikuu mzumbe Dk Arobogasti Musabila

TAMASHA LA AMKA KIJANA, TUIJENGE IRINGA YETU LAFANA MJINI IRINGA

Mkuu wa wilaya ya Iringa Mhe. Richard Kasesela akimtambulisha mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza (mwenye ushungi) huku mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza, Steve Nyerere akifuatilia kwa karibu wakati wa Tamasha la Amka Kijana, Tuijenge Iringa Yetu lililofanyika uwanja wa Mwembetogwa, Iringa mwishoni mwa wiki iliyopita.
Mkuu wa wilaya ya Iringa Mhe. Richard Kasesela (kushoto) akifurahia burudani iliyokuwa ikitolewa na msanii wa Muziki wa Singeli, Dulla Makabila wakati wa Tamasha la Amka Kijana, Tuijenge Iringa Yetu lililofanyika uwanja wa MwembeTogwa, Iringa mwishoni mwa wiki iliyopita.
 Msanii wa Bongo Fleva, Nuh Mziwanda nae hakuwa nyuma kutoa burudani. Mkuu wa wilaya ya Iringa Mhe. Richard Kasesela akizungumza na wana-Iringa waliojitokeza katika amasha la Amka Kijana, Tuijenge Iringa Yetu lililofanyika uwanja wa MwembeTogwa, Iringa mwishoni mwa wiki iliyopita. Mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza, Msanii wa Bongo Movies, Steve Nyerere ambao ndiyo waandaaji wa Tamasha la Amka Kijana, Tuijenge Iringa Yetu akizungumza machache na wakazi wa Iringa juu ya kutunza Amani, Upendo na Mshikamano wetu katika uwanja wa MwembeTogwa, Iringa mwishoni mwa wiki iliyopita.

Mkuu wa wilaya ya Iringa Mhe. Richard Kasesela akiwatambulisha wasanii wa Bongo Movie waliofika katika Tamasha la Amka Kijana, Tuijenge Iringa Yetu lililofanyika uwanja wa MwembeTogwa, Iringa mwishoni mwa wiki iliyopita. Mratibu wa Tamasha la Amka Kijana, Tuijenge Iringa Yetu, Msanii wa Bongo movies, Single Mtambalike (Rich Rich) akizungumza machache wakati wa tamasha hilo lililofanyika uwanja wa MwembeTogwa, Iringa mwishoni mwa wiki iliyopita. Msanii maarufu wa Bongo Movies Jacob Steven 'JB ' akieleza machache. Msanii maarufu wa Bongo Movies Jacob Steven 'JB ' akimtambulisha msanii mwenzake Weru Sengo. Msanii wa Kundi la Ze Komed akitoa burudani. Mchekeshaji maarufu, Mama Asha Boko akitoa burudani. Dj Choka nae alipata wasaa wa kutoa neno kwa wana-Iringa. Msanii wa Bongo Movies, Anti Ezekiel akiwasalimu wakazi wa Iringa.
Msanii wa Bongo Movies, Jackline Wolper toa burudani.
Wanamuziki wa bendi ya Fm Academia Wazee wa Ngwasuma wakitoa burudani.
Wasanii wa Bongo movies wakipata picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Iringa,  Richard Kasesela na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza na viongozi wengine wa Mkoa mara baada ya kumalizika kwa Tamasha la Amka Kijana, Tuijenge Iringa Yetu.

Comments

Popular posts from this blog

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.

AMANI YETU TUILINDE NAIBU WAZIRI CHANDE AZUNGUMZA KATIKA IJITIMAI JIJINI DODOMA