WANATAALUMA WAMUAGA MAREHEMU PROFESA SAMWEL MASELE ALIYEWAHI KUWA MKURUGENZI MKUU HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI


 Mwili wa aliyewahi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Taifa Muhimbili ukiwasili katika kiwanja cha Graduation Square MUHAS  ukisindikizwa na wanataaluma jana April 11, 2017 ambapo mazishi yamefanyika katika makaburi ya Kinondoni leo April 12, 2017 Jijini Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)

 Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Profesa Lawrence Museru (kulia) akiangalia mwili wa Marehemu Profesa Maselle ukishushwa toka katika gari maalumu lililokuwa limebeba mwili huo jana, wapili kulia ni Profesa Ayubu Magimba
 Mwili wa aliyewahikuwa Mkurugenzi Hospitali ya Taifa Muhimbili Ukiwasili katika kiwanja cha Graduation SQuare Muhas ambapo taratibu za kutowa heshima za mwisho zilifanyika jana April 11, 2017 na leo April 12, 2017 mwili huo unatarajiwa kupumzishwa katika makaburi ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam
 Wanataaluma mbalimbali wakiwa wanaushusha mwili wa mpendwa wao marehemu Profesa, Samuel Maselle kwa maandalizi ya kutowa heshima za mwisho jana
 Baadhi ya viongozi katika meza Kuu akiwemo Profesa, Ephata Kaaya (wa tatu kushoto) wapilikushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Profesa, Lawrence Museru na wa kwanza kushoto ni Profesa Ayub Magimba
 Baadhi ya wanafamilia na wana Taaluma wa Muhas

 Kaimu Mkuu wa Skuli ya Tiba, (MUHAS) Dokt, Erasto Mbugi akisoma wasifu wa Marehemu

  Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Profesa Lawrence Museru akisoma wasifu kwa niaba ya Hospitali ya Taifa na kutowa Rambirambi kwa niaba  ya wafanyakazi wa hospitali hiyo
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete akisoma wasifu wa Marehemu Maselle kwa niaba ya Taasisi hiyo
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mifupa, Muhimbili (MOI) Dokt, Respicious Boniface akisoma wasifu kwa niaba ya Taasisi hiyo na kutowa Rambirambi kwa niaba  ya wafanyakazi wake
 Ndugu wa Marehemu akishukuru kwa wote waliyojitolea kwa hali na mali kushirikiana na familia bega kwa bega kusaidia kuokoa maisha ya ndugu yao na hata mlipo sikia ndugu yetu katutoka hamkutuacha peke yetu na mmekuwa mstari wa mbele kufanikisha shughuli nzima za maandalizi ya kumsindikiza mpendwa wetu Profesa Maselle kuelelea katika nyumba yake ya milele na mmekuwa nasi mwanzo hadi kufikia tulipo fikia. nawashukuruni sana na mungu awabariki
 Sehemu ya wanataaluma mbalimbali
 Baadhi ya wana taaluma wakifatilia kwa umakini yaliyokuwa yakiendelea Chuoni hapo



 Aliyewahi kuwa Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Dr. Marina Njelekela akitowa heshima za mwisho kwenye jeneza lenye mwili wa aliyewahi kuwa Mkurungezi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Profesa, Samuel Maselle katika kiwanja cha Graduation SQuare Muhas 
 Waombolezaji wakitowa heshima za mwisho
 Mkurugenzi wa Uuguzi Hospitali ya Taifa Muhimbili, Agnes Mtawa (aliyeshika mwamvuli) akitowa heshima za mwisho katika jeneza lenye mwili wa aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Hospitali hiyo

 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mifupa, Muhimbili (MOI) Dokt, Respicious Boniface akitowa heshima za mwisho katika jeneza lenye mwili wa aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Hospitaliya Taifa Muhimbili

 Wanataaluma wakiubeba mwili wa marehemu Maselle kuuweka katika gari maalumu tayari kwa kuelekea nyumbani kwa marehemu Mbezi Beach
Mwili wa Marehemu Maselle ukiingizwa jana katika Gari

LAPF WATAMBULISHA HUDUMA YA UWEKAJI AKIBA KWA WANACHAMA WA HIARI

Kaimu Mkurugenzi wa Huduma kwa Wanachama Bw. Ramadhani Mkeyenge akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu dhana nzima ya utaratibu wa uwekaji akiba kwa hiari kwenye Mfuko wa Pensheni wa LAPF kwenye mkutano uliofanyika Makao makuu ya Mfuko mjini Dodoma .
Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF Bw. James Mlowe akizungumza na waandishi wa Habari mjini Dodoma kuhusu umuhimu wa matumizi ya teknolojia ikiwemo huduma za M-pesa na Tigo-pesa katika kuwafikia Watanzania walio wengi ili wajiunge na kuweka akiba kupitia “LAPF Jiongeze Scheme”.
Meneja mwenye dhamana na Skimu ya uchangiaji wa hiari (LAPF Jiongeze Scheme) Bi. Hanim Babiker akizungumzia taratibu mbalimbali zinazotakiwa kufuatwa ili kuweka akiba kwa njia ya M-pesa na Tigo-pesa wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari mjini Dodoma.
Afisa huduma kwa wanachama wanaoweka akiba kwa hiari (LAPF Jiongeze Scheme) Bw. Juma Venerando akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari jinsi Mfuko wa Pensheni wa LAPF ulivyojipanga kuendelea kuboresha zaidi huduma kwa wanachama.
Mwakilishi wa Kampuni ya Tigo Mkoani Dodoma Bw. Gideon Morris akizungumza na waandishi wa Habari jinsi kampuni hiyo ilivyojipanga kiteknolojia katika kuhakikisha ubora zaidi wa huduma zao za Tigo-pesa na hivyo kuwawezesha watanzania wote kuweka akiba ya hiari Kwenye Mfuko wa LAPF.
Mwakilishi wa Kampuni ya Vodacom Mkoani Dodoma Bw. Balikulije Mchome akizungumza na waandishi wa Habari jinsi kampuni hiyo ilivyojipanga kiteknolojia katika kuhakikisha ubora zaidi wa huduma zao za M-pesa na hivyo kuwawezesha watanzania wote kuweka akiba ya hiari katika Mfuko wa Pensheni wa LAPF.
Waandishi wa Habari kutoka vyombo mbalimbali wakifuatilia kwa makini maelezo mbalimbali yaliyotolewa kwenye utambulisho wa huduma za uwekaji wa akiba ya hiari kwa njia ya M-pesa na Tigo-pesa kwenye Mfuko wa Pensheni wa LAPF, mkutano uliofanyika mjini Dodoma.

RAIS DKT. MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA RELI YA KISASA STANDARD GAUGE KUTOKA DAR HADI MOROGORO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa pamoja na Mkewe Mama Janeth Magufuli akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa Standard Gauge itakayoanzia jijini Dar es Salaam hadi mkoani Morogoro na baadaye kuendelea hadi mikoa ya Kigoma na Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akiweka jiwe la msingi Ujenzi wa Reli ya Kisasa Standard Gauge itakayoanzia jijini Dar es Salaam hadi mkoani Morogoro na baadaye kuendelea hadi Kigoma na Mwanza.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia majina ya baadhi ya wataalamu mbalimbali waliohusika katika mchakato wa Ujenzi huo wa Reli ya Kisasa Standard Gauge itakayoanzia jijini Dar es Salaam hadi mkoani Morogoro na baadaye kuendelea hadi Kigoma na Mwanza. Wakwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hodhi ya Rasilimali za Reli (RAHCO) Masanja Kadogosa akiwa ameshika majina hayo.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akichota mchanga na kuweka kama ishara ya kushiriki katika ujenzi huo wa Reli ya Kisasa Standard Gauge itakayoanzia jijini Dar es Salaam hadi mkoani Morogoro na baadaye kuendelea hadi Kigoma na Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia kibao cha jiwe la msingi cha Ujenzi wa Reli ya Kisasa Standard Gauge itakayoanzia jijini Dar es Salaam hadi mkoani Morogoro na baadaye kuendelea hadi Kigoma na Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mabarawa, Mama Janeth Magufuli wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa RAHCO Masanja Kadogosa wakati akielezea kuhusu ujenzi wa Reli ya Kisasa Standard Gauge itakayoanzia jijini Dar es Salaam hadi mkoani Morogoro na baadaye kuendelea hadi Kigoma na Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amechuchumaa kwenye mfano wa Reli ya Kisasa (SGR) na Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mabarawa, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa RAHCO Masanja Kadogosa, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Miundombinu Profesa Norman Sigala mara baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Reli hiyo, wengine katika picha ni Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli pamoja na Hawa Ghasia (Mb).
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mabarawa wakati akipita katika katika ya mfano wa Reli hiyo itakayojengwa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wananchi waliohudhuria sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi Ujenzi wa Reli ya Kisasa Standard Gauge itakayoanzia jijini Dar es Salaam hadi mkoani Morogoro na baadaye kuendelea hadi Kigoma na Mwanza.
Mfano wa Reli hiyo ya Kisasa ya Standard Gauge SGR itakayojengwa kuanzia Dar es Salaam hadi Morogoro na baadae kuendelea hadi mikoa ya Mwanza na Kigoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Kaimu Mtendaji Mkuu wa RAHCO Masanja Kadogosa wakati akielekea kuweka jiwe la Msingi ujenzi wa Reli hiyo ya Kisasa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia kabla ya kuweka jiwe la Msingi ujenzi wa Reli hiyo ya Kisasa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Mufti Mkuu wa Tanzania Shekhe Abubakary Zubeiry mara baada ya kuweka jiwe la Msingi katika eneo la Pugu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza msanii Mrisho Mpoto mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika ujenzi huo wa Reli ya Kisasa Pugu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU.

Comments

Popular posts from this blog

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

AMANI YETU TUILINDE NAIBU WAZIRI CHANDE AZUNGUMZA KATIKA IJITIMAI JIJINI DODOMA

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.