JUKWAA LA KATIBA NA KATIBA MPYA

Mkurugenzi Mtendaji wa Jukwa hilo Hebron Mwakagenda,akizungumza mwanzoni mwawiki hii na wanahabari akiitaka Serikali ikamilishe mchakato wa katiba mpya iziangatie matakwa ya Watanzania na uhalisia wa mmchakato wenyewe



Nchi yoyote Duniani inayoongozwa kwa mujibu wa sheria ni lazima iwe na katiba yake ambayo itakuwa inamuongoza kila mtu au kiongozi anapotaka kufanya maamuzi yake yasiyokuwa ya kidikiteta hapo wanananchi watakuwa na imani nae .

Nchini Tanzania tulikuwa na katiba ambayo wengi walidai imepitwa na wakati  na utawala wa awamu ya nne ukatoa mamilioni ya fedha kutafuta maoni kwa ajili ya katiba mpya.
Kilichofanya watanzania wasipate katiba mpya  inadawa kujaza makada wengi wa chama cha mapinduzi CCM kwenye Bunge la kuipitisha katiba hiyo, matokeo yake ikashindikana  sasa tumekuwa taifa la ajabu fedha zimeliwa na katiba haipo iliyotalajiwa.

Jukwaa la Katiba limekuwa kisemeo la Watanzania wasiokuwa na kipaza sauti cha kusikika wanadai mwendelezo wa katiba yao ulioshindikana kipindi kile uendelee ili waondokane na katiba iliyojaa viraka.
Sheikh Juma Ali Maneno, akizungumza na mwandishi wa makala hii, aliwapongeza viongozi wa Jukwaa la Katiba kwa moyo wao wa kuendelea mazungumzo ya kuataka viongozi wa nchi hii wamuogope mungu ili wawaletee wananchi katiba yao ambayo itakuwa dira kwao waondokana na mambo ya kubahatisha na kutishwa na baadhi ya viongozi wenye kutaka kuambudiwa hata kama uwezo wa kiutendaji hawana.

 Na hivi sasa hata vyombo vyahabari vimeanza kuandamwa kuacha kuwafuata fuata wakubwa pindi wanapotekeleza mambo yao  hata kama kwawanananchi na vyombo vya habari wanaona hayafai


Historia ya vyombo vya habari baada ya Tanganyika kupata uhuru wake mwaka 1961 tunaelezwa kwamba   Serikali ya Tanganyika ilianza kujipanga kwa kuchukua hatua kadhaa  kuhakikisha inarejesha heshima ya wananchi wake waliokuwa wameonewa, wamenyonywa na kupuuzwa kwa miaka mingi ya utumwa wa ukoloni.

Katika mikakati hiyo mnamo mwaka  1967 Serikali ilikuwa chini ya Chama  TANU ilianzisha kile ilichokiita  Azimio la Arusha ikiwa na lengo la kuhakikisha njia zote za uchumi zinamilikiwa na umma kabla ya  mwaka 1970  aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Mwalimu Julius Nyerere  kutoa  sera mpya ya vyombo vya habari kupitia gazeti la The Standard (ambalo kwa sasa linaitwa  Daily News.

Katika sera  hiyo  ya vyombo vya habari ilivielekeza  vyombo vya habari nchini kuunga mkono falsafa ya Ujamaa na Kujitegemea na dhima kuu ikiwa na mambo matano.

Mambo hayo ni  kama ifuatavyo (i) Kuhabarisha wananchi kuhusu masuala yote muhimu ya ndani na nje ya nchi (ii) Kuelimisha, kufunza (iii) Kuwa kiungo cha mawasiliano ya serikali kwa wananchi (iv) Kuhamasisha wananchi katika masuala mbalimbali kama vile ukombozi wa majirani zetu waliokuwa chini ya ukoloni (v) Kukosoa kwa uhuru vitendo vyovyote vya viongozi wa chama au serikali ambavyo vinavyoenda kinyume cha misingi au maslahi ya nchi na kuburudisha.

Hata hivyo pamoja na sera hiyo kwa upande mmoja kuonekana kuwa ni nzuri, lakini ukiichunguza kwa upande wa pili wa shilingi, baada ya uhuru  Serikali iliendelea kubaki na sheria   zile zile za wakoloni za kudhibiti vyombo vya habari.

Moja ya sheria hizo ni ile ya magazeti ya mwaka  1976 au ile ya Shirika  la Habari Tanzania (SHIHATA) ya mwaka 1976 ambazo zote kwa pamoja  zililenga kudhibiti mfumo wa habari kwa namna ile ile wakoloni walivyokuwa wanafanya, japo kwa mitazamo tofauti.

Na hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haikuwa na vifungu vilivyotambua au kulinda dhima ya vyombo vya habari katika jamii. Aidha, hata mwaka 1984 pale vifungu vya haki za binadamu vilipoingizwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania ya mwaka 1977 bado vyombo vya habari havikutamkwa popote mbali tu na Ibara ya 18, kifungu cha (i) ambacho kilizungumzia haki ya kila mtu kuwa na maoni yake, ikiwa ni pamoja na uhuru wa kukusanya, kupokea na kusambaza taarifa kupitia chombo chochote cha habari bila kujali mipaka na kifungu cha (ii) kilichosema: kila mtu anayo haki ya kuhabarishwa kuhusu masuala muhimu kwa maisha yake yanayotokea ndani na nje ya nchi.

Vyombo vya habari kwa ujumla wake vilidhibitiwa na sera na sheria za vyombo vya habari, lakini pia mfumo uliojengwa katika falsafa ya Ujamaa na Kujitegemea na uliozingatia tunu za usawa, utu, umoja na uzalendo.
Vyombo vya habari vilichukuliwa zaidi kama taasisi za kutoa huduma na si biashara ya kutafuta faida kama ilivyo leo. Aidha umiliki wa vyombo vya habari ulikuwa ama chini ya serikali au taasisi.

Watu binafsi hawakuhamasika kuanzisha vyombo vya habari katika mazingira yaliyokuwapo. Falsafa ya sekta ya habari na mawasiliano ilikuwa: Mawasiliano kwa ajili ya maendeleo.

Hali hiyo ndiyo ipo hadi sasa  kutokana na kwamba Ibara  hiyo ya  18 ya Katiba inaendelea kueleza kwamba “bila kuathiri sheria za nchi, kila mtu ana uhuru wa kuwa na maoni, ingawa mwaka 2005 baada ya harakati mbaimbali zilizochukuliwa na  wadau wa masuala ya uhuru wa habari,  ilirekebishwa na ile sentensi ya: “bila kuathiri sheria za nchi…” iliondolewa.

Kwa hali hiyo inamaana kwamba pamoja na mabadiliko hayo kidogo  katiba  ya sasa ina sauti ya juu kuliko sheria nyingine ndogo katika kulinda haki ya kila mtu kuwa na maoni au kukusanya, kupokea na kusambaza taarifa, japokuwa bado ibara ya 30 inadhibiti uhuru huo.

Pamoja na hilo pia hadi sasa ndani ya katiba hiyo  bado kuna  sheria zinazokwamisha uhuru wa vyombo vya habari ikiwamo Sheria ya Magazeti ya 1976 ambayo, pamoja na mambo mengine, inampa waziri mwenye dhamana ya masuala ya habari madaraka ya kufungia gazeti lolote wakati wowote anapoona inafaa kufanya hivyo.

Sheria hiyo imekuwa ikipigiwa kelele na wadau mbalimbali wa habari na asasi za kijamii kuanzia mwaka 2001 ili ifanyiwe marekebisho na ile ya  utangazaji ya mwaka 1993 ili ziweze kwendana na wakati tuliopo.


Kutokana na kilio hicho Serikali kwa kushirikiana na wadau waliweza kufanikisha kukamilika mchakato huo mwaka 2003  ambao ulipewa jina la  Sera ya Habari na Utangazaji 2003 na mwaka  mwaka 2006 Serikali ilitaka kupeleka Muswada wa Haki ya Kupata Habari kama ilivyoelekezwa katika sera mpya lakini ukakataliwa na wadau wa tasnia hiyo baada ya kubaini makandokando yalikuwamo.
Hivyo wakaamua kukutana na kuanza mchakato mwingine wa kuwashirikisha wananchi ili kupata maoni juu ya sheria hiyo na baada ya mchakato huo wakaamua  kuandika mapendekezo ya miswada miwili na kuikabidhi serikalini.

Tangu mwaka 2009 mapendekezo ya wadau kuhusu muswada wa haki ya habari na huduma za vyombo vya habari yalipowasilishwa Wizara ya Habari, Utangazaji na Michezo yamekwamia pale, japo kila mara Serikali huahidi kuipeleka bungeni. Kupitishwa kwa muswada huo kuwa sheria kungelimaanisha kufutwa kwa sheria mbaya kama ile ya magazeti ya mwaka 1976 ambayo imekuwa ikitumika kufungia magazeti bila kufuata taratibu za kimahakama au hata kutoa sababu za kuridhisha kitaaluma.

Ikumbukwe kuwa sheria ya magazeti ya mwaka 1976 Namba. 1 ambayo inatakiwa kufutwa kutokana  na kukinzana na misingi ya demokrasia ya  uhuru wa vyombo vya habari pamoja na ya vyama vingi.

 Kinachojitokeza hapa ni kwamba serikali inaonesha sura  ya kupenda kuendelea na sheria zake  hizo za zamani inazoamini hazitaweza kutoa uhuru zaidi kwa wananchi wake kutoa  maoni, kujieleza, kujua na kupata kwa uhuru zaidi kile kinachopitia katika vyombo vya habari.
Na ili hali hiyo iweze kuondoka ni lazima kuundwa Katiba nyingine mpya ambayo itawapunguza makali baadhi ya watendaji wa serikali waliopewa dhamana ya kusimiamia vyombo kuchukua hatua kwa kukurupuka na kuvifungia vyombo hivyo bila kufanya uchunguzi wa kina.

Katiba na ifufuliwa sasa kwani wakati ni huu ili hapo badae pasitokee mungu watu wasiofuata sheria  wala katiba mungu ibaliki tanzania mungu libaliki Jukwaa la Katiba Tanzania.



Comments

Popular posts from this blog

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.

AMANI YETU TUILINDE NAIBU WAZIRI CHANDE AZUNGUMZA KATIKA IJITIMAI JIJINI DODOMA