BODI YA ZABUNI YA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YAIPA WIKI TANO KAMPUNI YA UJENZI YA KOBERG KUKAMILISHA UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAMISHNA WA UHAMIAJI, JIJINI D’SALAAM


Mwenyekiti wa Bodi ya Zabuni ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga (watatu kushoto), Katibu wa Bodi hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Manunuzi wa Wizara hiyo, David Mwangosi wakimsikiliza Mkuu wa Kitengo cha Majengo wa Idara ya Uhamiaji, Hamza Shabani (kushoto), wakati wajumbe wa Bodi hiyo walipotembelea nyumba za makazi za Makamishna wa Uhamiaji, Mtoni Kijichi, jijini Dar es Salaam. Bodi hiyo ilitoa wiki tano kwa Kampuni ya Ujenzi ya Koberg kukamilisha ujenzi wa nyumba hizo.

Katibu wa Bodi ya Zabuni, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia Mkurugenzi wa Manunuzi wa Wizara hiyo, David Mwangosi akiwafafanulia jambo Wajumbe wa Bodi ya Zabuni ya Wizara hiyo, wakati wajumbe hao walipofanya ziara ya kukagua ujenzi wa nyumba za makazi ya makamishna wa Uhamiaji zilizopo Mtoni Kijichi, jijini Dar es Salaam. Hata hivyo, Wajumbe wa Bodi hiyo walitoa wiki tano kwa Kampuni ya Ujenzi ya Koberg kukamilisha ujenzi wa nyumba hizo. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi hiyo, ambaye pia ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga.

Mwenyekiti wa Bodi ya Zabuni, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga (kushoto) akiangalia kabati la nguo katika moja ya chumba cha nyumba za makamishna wa Uhamiaji zilizopo Mtoni Kijichi, jijini Dar es Salaam. Wajumbe wa Bodi hiyo walizikagua nyumba hizo na kutoa wiki tano kwa Kampuni ya Ujenzi ya Koberg kukamilisha ujenzi.
Mkuu wa Kitengo cha Majengo wa Idara ya Uhamiaji, Hamza Shabani akiwaonyesha Wajumbe wa Bodi ya Zabuni ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, nyumba za makazi za makamishna wa Uhamiaji zilizopo Mtoni Kijichi, jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi hiyo, ambaye pia ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga. Wapili kulia ni Katibu wa Bodi hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Manunuzi wa Wizara hiyo, David Mwangosi, watatu kulia ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Uhamiaji, Peter Chogero, na kulia ni Mhasibu Mkuu wa Wizara hiyo, Edwin Makene.
Mhandisi wa Kampuni ya Ujenzi ya Koberg ambayo inajenga nyumba za makazi za Makamishna wa Idara ya Uhamiaji, Leonard Leonidace, akiwafafanulia jambo Wajumbe wa Bodi ya Zabuni ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, walipozitembelea nyumba hizo wakikagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba hizo, hata hivyo Wajumbe wa Bodi walitoa wiki kwa Kampuni hiyo kukamilisha ujenzi. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Zabuni, Wizara hiyo ambaye pia ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga, na wanne kulia ni Katibu wa Bodi hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Manunuzi wa Wizara hiyo, David Mwangosi.
Mwenyekiti wa Bodi ya Zabuni, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga (Katikati) na Katibu wa Bodi hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Manunuzi wa Wizara hiyo, David Mwangosi (wanne kulia), wakiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi hiyo, mara baada ya wajumbe hao kumaliza ziara yao ya kukagua ujenzi wa nyumba za makazi za Makamishna wa Idara ya Uhamiaji, zilizopo Mtoni Kijichi, jijini Dar es Salaam. Hata hivyo, Wajumbe wa Bodi hiyo walitoa wiki tano kwa Kampuni hiyo kukamilisha ujenzi wa nyumba hizo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.


Bodi ya Zabuni ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, imeipa muda wa wiki tano Kampuni ya Ujenzi ya Koberg Construction Co.Ltd kukamilisha ujenzi wa nyumba za makazi za Makamishna wa Idara ya Uhamiaji hapa nchini zilizoko katika eneo la Mtoni Kijichi jijini Dar es Salaam ambazo zitatumiwa na Makamishna hao.

Uamuzi wa Bodi hiyo umekuja baada ya Kampuni ya Koberg Construction ya nchini hapa kuonyesha kusuasua na kushindwa kukamilisha ujenzi wa nyumba hizo kwa wakati.

Bodi hiyo inayoongozwa na Mwenyekiti wake Kamishna wa Utawala na Fedha wa Jeshi la Magereza, Gaston Sanga na Katibu wake Bw. David Mwangosi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Manunuzi cha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, imefanya maamuzi hayo baada ya kufanya ukaguzi na kujionea hatua zilizofikiwa katika ujenzi wa nyumba hizo.

Kwa upande wake Katibu wa Bodi hiyo amesema kitendo cha Mkandarasi huyo kusuasua kukamilisha kwa wakati kazi ya ujenzi wa nyumba hizo ulioanza tangu mwaka wa Fedha wa 2014/2015 ndicho kilichoifanya Bodi ya Zabuni ya Wizara hiyo kuamua kutembelea eneo ambalo kazi ya ujenzi wa nyumba hizo unaendelea na kumpatia wiki tano tu kuhakikisha anakamilisha kazi hiyo.

SALAMU ZA PASAKA KUTOKA KWA MSTAHIKI MEYA WA JIJI LA DAR ES SALAAM KWA WAKAZI WA MKOA WA DAR ES SALAAM

 
Ndugu wananchi wa Jiji la Dar es Salaam.

Napenda kutumia nafasi hii kwanza kabisa kumshukuru mwenyezi mungu kwa kuniwezesha kuwa mzima hadi siku hii ya leo. Ni dhahiri kwamba mmekuwa pamoja tangu nilipochaguliwa kuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam. 


akini pia mmekuwa bega kwa bega na mimi Meya wenu wa Jiji, katika juhudi kubwa za kulifanya jiji letu kuwa la kuvutia. Hivyo nina kila sababu ya kuwashukuru na kuwapongeza sana.

Ushirikiano ambao mnaunyesha na kuendelea kuuonyesha unanipa matumani makubwa kwamba tuko pamoja katika kuhakikisha kwamba tunaleta mabadiliko makubwa katika jiji letu na hivyo kuondokana na changamoto mbalimbali zinazo likabili jiji letu. hivyo naomba tuendelee kushirikiana na kuzidi kuniombea Meya wenu niweze kufanya kazi ambazo mmenituma katika jiji letu la Dar es Salaam.

Ni wazi mnafahamu kwamba, maendeleo ya jiji letu hajawezi kuletwa bila ya nyinyi wannachi kuonyesha ushirikiano kwa viongozi wenu ambao mmetuchagua kuanzia ngazi za Mitaa, Kata, Halmashauri pamoja na jiji.


Ndugu wananchi wa Jiji la Dar es Salaam.

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imekuwa na mipango mingi mizuri ambayo imelenga kuboresha maendeleo ya wananchi wake. Miongoni mwa mambo ambayo niweka na kuendelea kusimamia ili kuhakikisha kwamba wakazi wa jiji la Dar es Salaam wanapata huduma mbalimbali za kijamii kwa uhakika.


Ndugu wananch wa Jiji la Dar es Salaam.

Hivi sasa tunaingia kwenye kipindi cha sikuu ya pasaka. Tunapoungana na wenzetu Wakristo katika kusherehekea Sikukuu ya Pasaka, niwaombe wakazi wa jiji la Dar es Salaam kuendeleza kushirikiana na vyombo vyetu vya usalama katika suala zima la uimarisha wa usalama wenu.

Vyombo vya usalama vimekuwa rafiki kwa kipindi chote jambo ambalo limefanya kupungua kwa matukio ya kiuhalifu ndani ya jiji letu.

Hivyo basi nitoe rai kwa wakazi wote wa jiji la Dar es Salaam, kusherehekea siku kuu hii kwa Amani na utulivu bila kuwepo kwa vurugu zozote. Salamu zangu za upendo katika sikukuu hii ya Pasaka ziwe chachu ya kuendelea kutunza amani katika jiji letu, huku mki hakikisha kwamba kila eneo ambalo watoto wenu watashiriki kwa namna moja ama nyingine kuwe na usalama wa uhakika. Tusijenge utamaduni wakukubali matukio ya kuvunja amani kwenye siku kuu maana hizi ni sherehe sio vita.


Ndugu wananchi wa Jiji la Dar es Salaam,

Mtakubaliana name kwamba, Siku kuu hii imekuja na neema ya mvua, ukizingatia ni jambo ambalo tulikuwa tukililia kwa muda mrefu sana ili kuondokana na hali ya ukame. Napenda kutumia fursa hii kuwataka wale wote ambao wapo maeneo ya hatarishi (mabondeni), kuanza kuchukua tahadhari mapema kabla ya kukumbwa na adha ya mafuriko.

Sote ni mashahidi kwamba, wakati wa mvua kama hizi kumekuwa na madhara makubwa ambayo hujitokeza kwa wale ambao huishi mabondeni. Hivyo kama jiji linampango mkakati wa kuboresha miundombinu ya maji ili kuepukana na adha hii ya mafuriko. lakini basi wakati jiji likiwa kwenye mkakati huo, tuchukue tahadhari mapema kabla ya kuleta maafa.


Ndugu wananchi wa jiji la Dar es Salaa.

Nimekuwa katika majukumu mbalimbali ya kitaifa kwa ajili ya kuwahudumia wananchi wetu. Nitoe rai kwa wananchi kushirikiana na viongozi mliowachagua ili kuweza kuwasilisha kero zenu sehemu husika ili mamlaka ziweze kushughulikia kero hizo mapema.

Aidha Ofisi ya Meya wa jiji imekuwa rafiki kwa wananchi wote katika kuhakikisha kwamba tunakuwa na Jiji ambalo linajali mahitaji mbalimbali ya wananchi wake hususani wafanyabiashara wadogowadogo, Bodaboda, Mama lishe, na makundi mengine mbalimbali.


Ndugu wananchi wa Jiji la Dar es Salaam.

Halikadhalika pia, napenda kuvipongeza vyombo vyote vya habari kwa mchango mkubwa ambao mnaonyesha wa kuhabarisha Umma wa wa Tanzania mambo mbalimbali yanayofanywa na jiji. na kwamba mmekuwa ni chachu kubwa ya kutangaza shughuli mbalimbali zinazofanywa na jiji. Niseme tu kwamba jiji la Dar es Salaam, linatambua mchango wenu mkubwa na kuwaomba muendelee kufanya kazi zenu kwa weledi mzuri na kwamba tuko pamoja na nyie.

Ndugu wananchi wa Jiji la Dar es Salaam.

Mwisho kabisa niwatakie maandalizi mema ya sikukuu ya Pasaka ,iwe na heri na fanaka kwa watu wote, na kwamba mapumziko haya ya siku tatu, muyatumie kwa kulijenga jiji lenu badala ya kulibomoa.



Mwisho kabisa napenda kuwatakia sikukuu njema

Mungu ibariki Tanzania , mungu libariki jiji la Dar es Salaam.

Imetolewa na Mstahiki Meya wa jiji

…………………….

Isaya Mwita Charles.

MKUU WA WILAYA YA KISHAPU AFANYA ZAIARA KATA YA MASANGA NA KUZUNGUMZA NA WANANCHI, APIGA MARUFUKU UUZAJI WA CHAKULA


Mkuu wa Wilaya Kishapu mkoani Shinyanga, Nyabaganga Taraba amepiga marufuku wananchi kuuza mazao ya chakula wanayovuna hususan mtama na badala yake waweke akiba. 
Taraba alipiga marufuku hiyo jana wakati akifanya ziara katika kata za Lagana, Mwamashele, Mwakipoya na Masanga baada ya kubaini kuwepo kwa baadhi ya wananchi kufanya biashara hiyo. 
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara katika kata ya Masanga alisema kuna baadhi ya watu huwahadaa na kununua mtama kwa bei ya juu hali inayowafanya wananchi wabaki bila chakula. 
“Nasikia hapa kuna baadhi watu wanapita kwenu wananchi na kununua debe moja la mtama kwa shilingi elfu ishirini na tano msidanganyie na kuuza wewkeni akiba,” alisisitiza mkuu huyo wa wilaya. 
Aidha alionya tabia ya baadhi ya watu kuuza mazao yakiwa shambani baada ya kukadiriwa kiasi cha mazao yao kabla ya kuyavuna aliwataka wananchi wakatae kufanya hivyo. 
Kwa upande mwingine aliwataka kuandaa mashamba yao mapema na kupanda mazao yanayohimili ukame yakiwemo mtama ili yaweze kustawi na kuwapa chakula. 
Taraba aliwataka wananchi hao kuwatumia wataalamu wa kilimo kwenye kata zao ili kupata ushauri wa kutumia mbegu zilizo bora ambazo zinaweza kuota na kukua kwa haraka.
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Nyabaganga Taraba (katikati) akizungumza na wananchi (hawapo pichani) katika mkutano wa hadhara kata ya Masanga. kulia ni Afisa Kilimo (Ubora wa mbegu), Maduhu Masunga 
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Nyabaganga Taraba (katikati) akizungumza na wananchi (hawapo pichani) katika mkutano wa hadhara kata ya Masanga. Wengine pichani kulia ni Afisa Kilimo (Ubora wa mbegu), Maduhu Masunga na Mwenyekiti wa kijiji cha Masanga, Gambishi Malele. 
Mwananchi wa kata ya Masanga akitoa kero yake kwa Mkuu wa Wilaya, Nyabaganga Taraba wakati wa mkutano wa hadhara. 
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Nyabaganga Taraba akizungumza na wajumbe aliowakuta wakifanya kikao cha kujadili maendeleo ya kata, Mwamashele alipokuwa katika ziara ya kutembelea kata tatu. 
Mwananchi wa kata ya Masanga akitoa kero yake kwa Mkuu wa Wilaya, Nyabaganga Taraba wakati wa mkutano wa hadhara. 
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Nyabaganga Taraba akizungumza na wananchi wa kata ya Masanga katika mkutano wa hadhara. Wengine pichani ni kuanzia kushoto ni Afisa Tawala wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Juvenalis Beyakwasho, Mtendaji Kata wa Masanga, John Zablon, na Mwenyekiti wa kijiji cha Masanga, Gambishi Malele. 
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Nyabaganga Taraba akizungumza na wananchi wa kata ya Masanga katika mkutano wa hadhara. Wengine pichani ni kuanzia kushoto ni Afisa Tawala wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Juvenalis Beyakwasho, Mtendaji Kata wa Masanga, John Zablon, na Mwenyekiti wa kijiji cha Masanga, Gambishi Malele. 

MAKALA YA KUMBUKIZI LA KUZALIWA MWALIMU NYERERE


Na Judith Mhina-MAELEZO

Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ulikuja hapa duniani Aprili 13, 1922 kupitia kwa Mpendwa Marehemu Bibi Mgaya wa Buritho kama zawadi kwa nchi ya Tanzania.

Mwalimu tunamshukuru Mungu kwa kutupa wewe ambaye umeitendea mambo makubwa Tanzania, Afrika na Dunia kwa ujumla.

Mwalimu wakati nakumbuka kuzaliwa kwako nimepata fursa ya kuangalia kazi ulizozifanya mara baada ya kuacha madaraka ya Urais na kujikita katika kazi kuu tano; Mosi pamoja na kubaki na kofia moja ya Uenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ya kuimarisha Chama na alianza maandalizi ya kukabidhi Uenyekiti huo kwa Rais aliyepokea madaraka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye alikuwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi.

Pili, mwaka 1986 baadhi ya Viongozi wa nchi za Kusini mwa Dunia, walikuomba kuanzisha Tume ya Uchambuzi wa maendeleo ya nchi za Kusini tangu miaka 30 iliyopita na kuweza kuona hatua za maendeleo na changamoto zilizopo katika mataifa hayo na mapendekezo ya nini kifanyike ili kuboresha ustawi wa wananchi.

Mwalimu Nyerere alikubali jukumu hilo, ndipo alianza kutembelea nchi 19 katika Bara la Asia na Marekani ya Kusini kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa  majukumu hayo mapya. Safari ya kutafuta maoni hayo ilikuwa ni pamoja na  kupata uthibitisho wa kuwaelewesha wananchi na nchi hizo kuhusu majukumu ya Tume na aina ya maoni yanayokusanywa.

Kazi hiyo aliifanya kwa miaka mitatu na kutoa ripoti kuwa nchi za Kusini zifanye maendeleo yao yenyewe yalenge maslahi ya wananchi walio wengi kwa kielelezo kuwa ili nchi za Afrika ziweze kupiga hatua za maendeleo ni vyema ziwe na mshikamano kama zinahitaji kushindana na nchi za Kaskazini.

“Nchi za Kusini zishirikiane kibiashara, kwa kuwa nchi za Kusini zina mazoea ya kufanya biashara na nchi za Kaskazini lakini hakuna utaratibu mzuri wa nchi za Kusini kufanya biashara wenyewe kwa wenyewe, au hata katika uwekezaji rasilimali” alisema Mwalimu Nyerere.

Aidha, Mwalimu Nyerere alisema Wataalam wengi wako Kusini lakini nchi za Kusini zinatafuta wataalam kutoka Kaskazini, hivyo ni wajibu wa nchi za Kusini kujenga na kuimarisha ushirikiano wa pamoja baina yao.

Tatu, Mwalimu alianzisha kituo cha muda cha Nchi za Kusini pale Geneva ambapo Mwalimu na Viongozi wengine walifanya kazi kwa muda wa miaka miwili, jukumu lao likawa kuelezea shughuli za maamuzi na mapendekezo ya Tume.

Nne, kuanzisha Ofisi ya kudumu ya Nchi za Kusini pale Geneva kwa ajili ya Mataifa hayo kutoa hoja kupitia vuguvugu la nchi za kundi la 77 ambazo hazikuwa na chombo cha kuwasaidia kupaza sauti zao.

Mwalimu akapokea jukumu hilo na kuanzisha Ofisi ya kudumu ambayo ilikuwa chombo cha Serikali badala ya chombo cha kiraia na kuhusisha nchi 49 ambazo ziliweka sahihi, pamoja na nchi kubwa ulimwenguni ikiwemo India, Brazil na Afrika ya kusini.

Tano, alikuja na wazo la kuanzisha Taasisi ya Mwalimu Nyerere, hatua iliyotokana na harakati za kazi yake ya kuunganisha nchi za kusini, ambapo alitaka taasisi hiyo kufanya kazi zake katika ukanda wote wa nchi za Bara la Afrika.

Miongoni mwa kazi hizo ni pamoja na kuangalia maendeleo ya watu, kupitia dhana ya umoja na ushirikiano miongoni mwao.

Nakumbuka hotuba ya Mwalimu Nyerere aliitoa mwezi Februari mwaka 1960, akiwa Rais wa chama cha Tanganyika African National Union (TANU) ,  alikaribishwa nchini Marekani katika Kongamano la Afrika katika Chuo cha Wellesley Massachusetts kuongelea kuhusu “Nafasi ya Afrika Duniani” .

Katika hotuba hiyo, Mwalimu alizungumzia hatua mbalimbali za ukombozi wa Bara la Afrika, mchango wa Waafrika katika Mataifa ya Ulaya na Marekani. Mwalimu alilisemea Bara la Afrika Kama Bara la matumaini kwa ubaguzi wa rangi.

Mwalimu alisisistiza kwa kusema “Muda utafika ambapo Marekani na Ulaya Magharibi watajisikia vibaya jinsi walivyoitumia Afrika” huku akitolea mifano ya mateso na manyanyaso waliyoyapata Waafrika ikiwemo vita vya Mau Mau nchini Kenya, vifo vya watu wa kabila la Waherero nchini Namibia, vita vya Majimaji nchini Tanzania.

Hotuba hiyo ilikuwa ya kwanza kwa Mwalimu Nyerere kuchapishwa kimataifa, hakika imeonyesha kwa dhati, Mwalimu hata kabla ya Uhuru alitambua nafasi ya umoja katika kupigania uhuru wa Bara la Afrika.

Aidha, ndoto hii ya umoja alisafiri nayo katika kujenga Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Nafasi ya Uenyekiti Jumuiya wa Nchi zilizo mstari wa mbele katika Ukombozi Kusini mwa Afrika, Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na nyingine nyingi.

Taasisi ya Mwalimu Nyerere dhumuni lake kuu ni kuendeleza Amani, Umoja na Utulivu wa Maendeleo ya pamoja Barani Afrika. Mwalimu alikuwa muanzilishi na Mweneyekiti wa kwanza wa Bodi ya Wadhamini wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere.

Septemba 14, 1996 alikaribishwa Kilimanjaro hoteli kuhutubia na kuzindua Taasisi ya Mwalimu Nyerere. Umuhimu wa Umoja, umuhimu wa ukubwa wa soko, Amani baina ya nchi ndani na nje ya nchi na Maendeleo katika Afrika.

Alipata fursa ya kukutana na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuwaeleza juu ya Taasisi hiyo na madhumuni yake. Katika kipindi hiki Mwalimu alikuwa msuluhishi wa mgogora wa Burundi.

Mwalimu leo ungetimiza miaka 95 tangu kuzaliwa, kimwili hatupo pamoja nawe, lakini fikra zako, mitazamo yako, utendaji wako bado ni dira na muelekeo wa Taifa letu Daima tutazifuata. Hakika siku ya leo ni siku muhimu sana kwa nchi yetu. Mungu ibariki Tanzania Mungu ibariki Afrika. 

MFUMO WA STAKABADHI GHALANI .

Jovina Bujulu- MAELEZO

Kuwepo na mfumo wa stakabadhi ghalani kumekuwa ni mkombozi pekee kwa wakulima wadogo na wa kati kwa kuwawezesha kupata bei nzuri ya mazao yao, ukilinganisha na bei zilizokuwa zinatolewa na wafanyabiashara wanaponunua mazao yakiwa shambani kwa kutumia vipimo ambavyo sio sahihi.

Taarifa iliyotolewa na bodi ya usimamizi wa Stakabadhi za Ghala imesema kuwa kabla ya mfumo huo kuanza wakulima walikuwa wakipunjwa bei ya mazao na wafanyabiashara na kutolea mfano zao la korosho ambapo katika msimu wa 2015/2016, kilo moja ya korosho ilinunuliwa kwa shilingi 2900 na msimu wa 2016/2017 bei ilipanda na kufikia shilingi 4,000 kwa kilo ambazo ni sawa na ongezeko la asilimia 15.9

Mfumo huo umewanufaisha wakulima kwa kutumia ghala ambazo ziliachwa kwa muda mrefu bila matumizi ambazo zimekuwa na tija kwa wakulima.

Kupitia ghala hizo zenye ujazo wa kuanzia tani 200 hadi 5000 na kuendelea wameweza kuhifadhi mazao yao vizuri na kwa ubora unaotakiwa kwa matumizi ya sasa nay a baadaye.

Aidha, mfumo huo umeongeza ajira kwa wakina mama na vijana hasa katika maeneo ya kuchambua, kupokea na kupanga mazao ghalani. Vijana wengi wameajiriwa kwa kazi ya kushusha, kupanga na kupakia mazao na wameweza kujiajiri katika kilimo baada ya kuona mfumo huo unavyofanya kazi vizuri na kuwa na uhakika wa soko la mazao yao.

Wakulima pia wamepata mafanikio kwa kuwa na uhakika wa vipimo vya mazao yao yanayohifadhiwa ghalani kupimwa kwa kilogramu na si vinginevyo ambapo kabla ya mfumo huo wakulima walikuwa wakiibiwa mazao yao kutokana na matumizi ya vipimo ambavyo si sahihi.

Kwa kuhifadhi mazao yao katika ghala zenye leseni, wakulima wamekuwa wanatumia mazao hayo kama dhamana ya kupata mikopo kutoka katika taasisi mbalimbali za fedha. Hii imewezekana kutokana na wakulima hao kujiunga katika umoja kupitia vikundi au vyama vya ushirika .

Wafanyabiashara pia wameneemeka na mfumo huu, ambapo kwa sasa wameweza kupunguza gharama za kufuata mazao maeneo mbalimbali mazao yanapatikana kwa wingi badala yake mazao hayo wanayapata katika eneo moja kkwenye ghala zilizosajiliwa na hivyo kuondoa hatari ya kuibiwa pesa zao na madalali wasio waaminifu.

Mfumo huo pia umekuwa na faida kwa bodi za mazao katika kuandaa bajeti za mahitaji ya pembejeo na kuongeza ili kuboresha na kuongeza uzalishaji.

Aidha, mfumo huo umechochea na kuharakisha uanzishwaji wa soko la bidhaa nchini, kutokana na kuwepo kwa bidhaa zenye ubora na zinazopatikana kwa wakati. Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala, inatoa wito kwa wakulima kuunga mkono uhamasishaji wa matumizi ya soko hilo ili kuongeza tija na kasi ya kukuza biashara ya mazao ya kilimo hapa nchini.

Mfuko wa Stakabadhi Ghalani ulianza mwaka 2000 ukifadhiliwa na Mfuko wa Kimataifa wa Bidhaa. Lengo la mfuko huo ni kuwezesha wakulima kufaidika na ongezeko la bei katika msimu wa mazao, kuongeza mapato ya wakulima na kuboresha kipato chao ikiwa ni pamoja na kuwapa wakulima nguvu ya soko kwa kuhamasisha utumiaji wa vikundi vya wakulima na ushirika.

TUKITAKA NCHI YA VIWANDA TUPIGE VITA DAWA ZA KULEVYA-ASKOFU BANZI.


ASKOFU wa Jimbo Katoliki la Tanga, Mhashamu Anthony Banzi akizungumza na wanafunzi kutoka shule mbalimbali Jijini Tanga wakati wa uzinduzi wa Juma la Elimu wilaya ya Tanga ambapo kiwilaya lilifanyika kwenye shule ya Sekondari Tanga Don Bosco iliyopo eneo la Maweni jijini Tanga inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Tanga.
ASKOFU wa Jimbo Katoliki la Tanga, Mhashamu Anthony Banzi wa pili kulia  akimkiliza mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule hiyo wakati alipokuwa akifafanua jambo
ASKOFU wa Jimbo Katoliki la Tanga, Mhashamu Anthony Banzi katikati akionyesha jambo na Sista ambaye anafanya kazi kwenye shule hiyo
ASKOFU wa Jimbo Katoliki la Tanga, Mhashamu Anthony Banzi amesema iwapo Serikali inataka nchi ya viwanda hawana budi kuweka msukumo mkubwa kwenye kupiga vita dawa za kulevya vitendo ambazo zimechangia kwa asilimia kuwaharibu vijana wengi hapa nchini. 

Banzi aliyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Juma la Elimu wilaya ya Tanga ambapo kiwilaya lilifanyika kwenye shule ya Sekondari Tanga Don Bosco iliyopo eneo la Maweni jijini Tanga inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Tanga. 

Alisema ili kutimiza azma hiyo ambayo ni muhimu kwa ukuaji wa uchumi wa  nchi lazima kuwepo na juhudi kubwa za kuuteketeza mtandao wa dawa za kulevya hapa nchini uliyoharibu vijana wengi ambao wangekuwa nguvu kazi  kubwa ya Taifa la kesho. 

“Kama tunataka kuifanya nchi kuwa ya viwanda maana yake kila mmoja apate elimu ya madhara ya dawa za kulevya lengo kubwa likiwa kuliondoa tatizo hilo kwa vijana ambalo limekuwa likipoteza nguvu kazi ambayo ingeweza kutumika katika shughuli mbalimbali lakini pia kuwepo kwa mapambano ya kupiga vita hali hiyo “Alisema. 

“Lazima kuwepo kwa dhamira ya dhati na mipango ambayo itawezesha kuutokomeza mtandao wa dawa za kulevya unaoangamiza vijana wengi ambao wangewezesha kufanya shughuli za uzalishaji mali na kujiingizia kipato halali na kuendesha maisha yao bila kuwa tegemezi “Alisema Askofu Banzi. 

“Vijana tuachane na matumizi ya dawa za kulevya ambayo imekuwa chanzo kikubwa cha kuharibu vijana ili kuendana na sera ya maendeleo ya viwanda kwa kuyapiga vita”Alisema. 

Akizungumzia suala la utunzaji wa mazingira,Askofu Banzi aliitaka
jamii kuacha kukata miti ovyo,kuchimba mahandaki ambayo kwa asilimia kubwa yamekuwa yakichangia uharibifu wa mazingira. “Kwani suala la ukataji miti ovyo limekuwa tishio kubwa hapa nchini na kuifanya kugeuka jangwa kitendo ambacho kimeweza kuchangia uharibifu mkubwa wa mazingira kwa jamii hivyo lazima tuachana na jambo hilo“Alisema. 

Awali akizungumza Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Don Bosco Gregory Mhuza alisema waliamua kupanda miti ili kuhakikisha wanatunza mazingira ambayo ni muhimu kwa jamii. 

“Sisi kama shule leo hii tumepanda miti lakini tutahakikisha
tunaitunza na kuilinda kwa vizazi vya sasa na vijazo ili kuiepusha
nchi yetu kukumbwa na janga “Alisema. 

Naye Mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi Maweni,Wales Janga alisema uzinduzi wa Juma la Elimu kwa kupanda miti katika shule hiyo ni ishara ya kuthamini uwepo wa mazingira kutokana na usemi usemao tunza mazingira yakutunze hivyo jamii haina budi kufanya hivyo ili kuendena na suala hilo.

“Pamoja na kupanda miti pia tutatembelea maabara ya ufundi kwani shule hii ni shule ya Ufundi ili tuweze kuona namna vijana wetu wanajifunza katika masomo yao ya ufundi kuelekea Tanzania ya Viwanda ya Mwaka 2025 “Alisema. 

Alisema kauli mbiu hiyo inalenga kuikumbusha jamii majukumu yake katika suala zima la elimu duni kwani baadhi yao wamelipokea suala la elimu bila malipo tofauti na kujisahau kuwa wao ni mdau namba“Alisema.

Comments

Popular posts from this blog

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.

AMANI YETU TUILINDE NAIBU WAZIRI CHANDE AZUNGUMZA KATIKA IJITIMAI JIJINI DODOMA