TBL NA TUICO WATILIANA SAHIHI MKATABA BORA WA MASLAHI YA WAFANYAKAZI

 Mkurugenzi Mtendaji wa TBL ,Roberto Jarrin (kulia) na katibu Mkuu wa TUICO, Boniface G Nkakatisi (kushoto) wakitiliana saini mkataba wa hiyari wa maboresho ya maslahi ya wafanyakazi wa TBL.Katikati ni Naibu waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana,Dk. Milton Mahanga.

 Naibu Waziri wa Kazi,Ajira na maendeleo ya Vijana, Dk.Milton Mahanga katikati, akipokea mkataba wa hiari wa maboresho ya wafanyakazi wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL),muda mfupi baada ya kusainiwa jana kati ya Mkurugenzi wa Mtendaji wa kampuni hiyo na Katibu Mkuu wa TUICO,Boniface G.Nkakatisi katika hafla iliyofanyika katika kiwanda cha Mwanza.

 Dk Milton Mahanga, mwenye tai ya michirizi ya rangi nyekundu akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa TBL tawi la Mwanza.Wanne kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Roberto Jarrin na kulia kwa Naibu Waziri ni Katibu Mkuu wa TUICO< Boniface G.Nkakatis na wa Kwanza kushoto ni Meneja wa TBL Mwanza, Raymond Richmond.

 Naibu Waziri wa Kazi,Ajira na Maendeleo ya Vijana, Dk.Milton Mahanga wa kwanza kushoto akitembelea kiwanda cha Bia cha TBL Mwanza na wa pili mbele( mwenye kofia nyeupe), ni Meneja wa Kiwanda hicho,Raymond Richmond .

 Naibu Waziri wa Kazi,Ajira na Maendeleo ya Vijana, Dk.Milton Mahanga, mwenye tai ya michirizi myekundu akitoka kutembelea kiwanda cha bia cha TBL Mwanza jana. Mbele yake ni Meneja wa kiwanda hicho, Raymond Richmond,mwenye kofia nyeupe.

.Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia (TBL),Roberto Jarrin,akitoa maelezo juu ya shughuli za uzalishaji wa kampuni hiyo ,kwa Naibu Waziri wa Kazi,Ajira na Maendeleo ya Vijana, Dk.Milton Mahanga (mwenye sutio na tai ya michirizi ya rangi nyekundu), alipotembelea kiwanda cha kaumpuni hiyo cha Jijini Mwanza jana.

Mkurugenzi wa Uhusiano wa TBL, Stephenus Kilindo,akisalimiana na Naibu Waziri wa Kazi,Ajira na Maendeelo ya Vijana, Dk.Milton Mahanga,alipotembelea kiwanda Mwanza kinachomilikiwa na kampuni hiyo ya bia.Wa kwanza kushoto ni Meneja Rasilimali watu wa TBL, David Magese
 Naibu Waziri wa Kazi,Ajira na Maendeleo ya Vijana, Dk.Milton Mahanga na Mkurugenzi Mtendaji wa TBL, Roberto Jarrin (kulia),kulia kwa Naibu Waziri ni Katibu mkuu wa TUICO, Boniface G.Nkakatisi wakimsikiliza Meneja wa TBL Mwanza, Raymond Richmond (hayupo pichani),akitoa maelezo juu ya uzalishaji wa kampuni hiyo jana.

 Meneja wa TBL Mwanza, Raymond richmond,akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Kazi,Ajira na Maendeleo ya Vijana, Dk.Milton Mahanga,juu ya shughuli za uzaliashaji wa kiwanda hicho, alipokitembelea jana.

 Roberto Jarrin Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia (TBL) akizungumza na wafanyakazi wa  kampuni hiyo jijini Mwanza jana, mara ya baada ya kutiliana saini mkataba wa hiari wa kuboresha maslahi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo.Kulia kwake ni Naibu Waziri wa Kazi, ajira na Maendeleo ya Vijana, Dk.Milton Mahanga na wa tatu kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa TUICO. Boniface G.Nkakatisi na wa pili kutoka kushoto ni Naibu Katibu MkuuTUICO, Salim Salehe .


Comments

Popular posts from this blog

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

AMANI YETU TUILINDE NAIBU WAZIRI CHANDE AZUNGUMZA KATIKA IJITIMAI JIJINI DODOMA

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.