Covenant Bank yatoa msaada wa nyumba
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Covenant
Bank Balozi, Salome Sijaona akikata utepe, kuashilia uzinduzi Rasmi wa Nyumba
aliyokabidhiwa Salome Mhando ambaye alitelekezwa na mume wake baada ya
kujifungua watoto mapacha mfurulizo hadi kufikia sita na kukosa Mahali pa
kuishi, Covenant Bank imemkabidhi nyumba hiyo ambayo ataimiliki yeye mwenyewe
pamoja na thamani za ndani na Bima ya Matibabu kwa Mwaka mzima. Anaeshuhudia ni
mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Sabetha Mwambenja.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Covenant
Bank Balozi, Salome Sijaona akikata utepe, kuashilia uzinduzi Rasmi wa Nyumba
aliyokabidhiwa Salome Mhando ambaye alitelekezwa na mume wake baada ya
kujifungua watoto mapacha mfurulizo hadi kufikia sita na kukosa Mahali pa
kuishi, Covenant Bank imemkabidhi nyumba hiyo ambayo ataimiliki yeye mwenyewe
pamoja na thamani za ndani na Bima ya Matibabu kwa Mwaka mzima. Anaeshuhudia ni
mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Sabetha Mwambenja.
Mama wa
Mapacha sita anunuliwa nyumba
Alijifungua mapacha mfurulizo na mume kumkimbia
Dar es Salaam 27 Januari 2015 . . . . Baada ya kujifungua watoto mapacha mfululizo na
kufuatiwa na kitendo cha kutelekezwa na mume wake huku akiwa hana sehemu ya
kuishi, Hatimaye Salome Muhando amenunuliwa na kukabidhiwa nyumba na
Covenant Bank ambayo ataishi yeye na watoto wake.
Salome ,
mwenye watoto sita mapacha alitelekezwa na mume wake baada ya kujifungua
mapacha mara tatu mfululizo na kusababisha kukosa sehemu maalum ya kukaa
yeye pamoja na watoto wake ambapo baada ya kutelekezwa msamaria mwema
alijitolea kumhifadhi katika shamba lake
lililopo eneo la
Mabwepande.
Baada ya kusikia
kilio cha mama huyo kupitia vyombo vya habari Covenant Bank, ilijitolea
kumnunulia nyumba mama huyo ambayo ataimiliki yeye moja kwa moja na kumpatia
mtaji wa biashara ambao utamsaidia kuenesha maisha yake ya kila siku.
Akizungumza na
waandishi wa habari, punde baada ya kukabidhi nyumba hiyo Mwenyekiti wa Bodi ya
Wakurugenzi wa Benki hiyo Balozi, Salome Sijaona, amesema baada ya kuona mateso
ambayo mwanamke huyo amekuwa akiyapata kwa kukosa makazi , Chakula na
mahitaji mengine ya kibinaadamu waliona ni vyema benki yake kujitolea kumsaidia
ikiwa ni katika sehemu moja ya kutimiza majukumu yake ndani ya jamii.
“Tumeguswa sana na mateso ambayo
amekuwa akiyapata Bi. Salome Mhando, yeye pamoja na watoto wake baada ya
kutelekezwa na mume wake kwa kigezo ha kuzaa watoto mapacha mfurulizo,
tuliguswa na kuamua kujitolea kumnunulia nyumba ambayo ataimiliki yeye
mwenyewe.” Alisema Balozi, Sijaona na kuongeza kuwa.
“Nyumba hii
tumemkabidhi pamoja na samani za ndani ya nyumba ambazo zitamuwezesha sasa
kuishi maisha ya amani, na furaha akiwa kama
wanawake wengine na kufurahi pamoja na watoto wake.”
Naye Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki hiyo Sabetha Mwambenja amesema kuwa pamoja na kumkabidhi
nyumba mama huyo pia Benki hiyo, imempatia Bima ya Matibabu kutoka AAR ambayo itamsaidia kupata Matibabu yeye pamoja na
watoto wake wote.
“Pamoja na
kumpatia nyumba Salome pia tunampatia Bima ya Matibabu ambayo
itamuwezesha yeye na watoto wote kutibiwa katiba Hopitali zote zilizo mahali
popote nchini, Tuna uhakika sasa atakuwa na uhakika wa afya yake na watoto wake
katika kipindi chote hivyo atakuwa na nafasi ya kufanya shughuli zake za
uzalishaji kwa amani., Alisema Mkurugenzi huyo
Kwa Upande wake
Salome , aliwashukuru Covenant Bank kwa kujitolea kumsaidia na sasa ana uhakika
wa maisha yeye pamoja na watoto wake.
“Ninawashukuru sana Benki ya Covenant kuniwezesha kumiliki nyumba yangu
ninawashukuru sana na ninaomba waendelee na moyo
huo wa kuwasaidia kina mama wenye matatizo kama
haya kwa sababu siko peke yangu,” alisema na kuongeza,
“ Kina mama
tumekuwa na wakati mgumu sana
katika ndoa zetu hususai katika masuala ya uzazi, Ninawashukuru watu wote ambao
walijitolea kunisaidia chakula na nguo katika wakati wote ambao nilikuwa sina
sehemu maalum ya kukaa, hadi sasa ninamiliki nyumba yangu. Alihitimisha Salome.
Comments
Post a Comment