Maajabu uchaguzi Serikali za Mitaa
Wasafiri wa mikoani wakiwa wamekwama katika stendi kuu ya mabasi unbungo jijini Dar es Salaam, baada ya kukosa usafiri mabasi yameadimika katika stendi hiyo kuelekea kwenye sikukuu ya mwaka mpya na Xsmasi
Baadhi yao wakitumia mabasi yanayotumika kwa daladala jijini Dar es salaam kama linavyosomeka mbele
Stendi ilicyokaukiwa na mabasi kama inavyoonekana katika picha,
UPIGAJI KURA WA AWAMU YAN PILI JIJINI DAR
Askari wakisimamia upigaji kura waawamu ya pili katika kituo cha Ali maua Kinondoni
Mpgakura akimalalmikia Askari baada ya jina lake kuonyesha limeshapigiwa kura huku yeye akiwa ndiyo anafika kituoni
Wapiga kura wakiwa wamejipanga kuingia sehemu ya kupigia kura kituo cha Chuo kikuu huria cha Tanzania Kinondoni
Ukawa na CCM, wakipashana
Askari akiwatuliza
Wakipashana
Akipiga kura kituo cha Buguruni
Wakihakiki majina yao
Baadhi yao wakitumia mabasi yanayotumika kwa daladala jijini Dar es salaam kama linavyosomeka mbele
Stendi ilicyokaukiwa na mabasi kama inavyoonekana katika picha,
UPIGAJI KURA WA AWAMU YAN PILI JIJINI DAR
Askari wakisimamia upigaji kura waawamu ya pili katika kituo cha Ali maua Kinondoni
Mpgakura akimalalmikia Askari baada ya jina lake kuonyesha limeshapigiwa kura huku yeye akiwa ndiyo anafika kituoni
Wapiga kura wakiwa wamejipanga kuingia sehemu ya kupigia kura kituo cha Chuo kikuu huria cha Tanzania Kinondoni
Ukawa na CCM, wakipashana
Askari akiwatuliza
Wakipashana
Akipiga kura kituo cha Buguruni
Wakihakiki majina yao
* Maajabu
uchaguzi Serikali za Mitaa
Wapigakura wakuta majina yametumika
*Mkurugenzi Ilemela awatibua Chadema
Dar na Mwanza
HAYA ni maajabu. Ndivyo unavyoweza kusema
baada ya wapiga katika kituo cha Shule ya Msingi Mwenge, Kinondoni jijini Dar es Salaam kufika kituoni na kukuta majina yao yakionyesha tayari
wamepiga kura.
Hali hiyo, ilisababisha kuibuka vurugu
kubwa ambazo zilisababisha upigaji kura katika uchaguzi huo wa marudio, kusitishwa
kwa muda.
Msimamizi wa uchaguzi katika kituo hicho, Nasoro
Kichuma alisema uchaguzi huo ulianza vizuri, lakini kadrii muda ulivyozidi
kwenda wapiga kura wengi walishangazwa namna majina yao yalivyotumiwa na watu wasiofahamika.
“Ni jambo la kushangaza kuona mtu anafika
kituoni kupiga kura halafu anakuta jina lake
limetumiwa, yaani inaonesha tayari
amekwishapiga kura … hali hii inazidisha wananchi kuwa na hasira na kushindwa
kutumia haki yao
ya msingi ya kidemokrasia kuchagua viongozi wanaowataka,”alisema Kichuma.
Mbali ya tukio hilo,
hali ilikuwa mbaya zaidi katika vituo vya Ali Maua, Kata ya Kijitonyama na Kituo
cha Mnyamani Buguruni, ambako eneo hilo
liligeuka uwanja wa masumbwi kati ya wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na
Chama cha Wananchi (CUF).
Watu wanaodaiwa kuwa wafuasi wa CCM,
walipigana ngumi kavu kavu na vijana
wanaodaiwa kutoka CUF kwa kile kilichodaiwa kuwa wapiga kura wengi waliofika
kituoni hapo ni mamluki.
Msimamizi wa uchaguzi Kituo cha
Mnyamani-Buguruni, Jumanne Muhanji alisema tangu kufunguliwa kwa kituo hicho
asubuhi wafuasi walikuwa wakilumbana.
Alisema baada ya hali kuwa mbaya zaidi,
polisi walilazimika kuingilia katika kutuliza hali hiyo.
KITUO CHA ALI MAUA
Katika kituo hicho, vurugu zilitawala baada
ya watu 30 wanaodhaniwa kuwa mamluki wa CCM kufika kwa ajili ya kupiga kura.
Msimamizi msaidizi wa kituo hicho, Abdalah
Mkenge alisema uchaguzi ulianza vizuri
asubuhi kwa kuweka utaratibu mpya wa namba tofauti na uchaguzi uliopita wa
kusoma majina.
Alisema licha ya kutumika utaratibu huo,
bado changamoto ya mamluki ilijitokeza kwani wengi wao walidaiwa kufika kituoni
hapo wakiwa katika gari aina ya Noah, kitendo kilichoamsha hasira kutoka kwa
wafuasi wa CUF.
Hali hiyo, ilitulizwa baada ya polisi
waliokuwa na silaha na mabomu ya machozi kufika.
Hali ya usalama katika kituo cha vingunguti
ilionekana kuwa tulivu, baada ya polisi wengi kuonekana eneo hilo.
Hali ya kutoaminiana kwa wapiga kura
ilitawala, huku wengi wakishindwa kuona majina yao kwenye
ubao wa matangazo.
Katika kituo cha Misewe, uchaguzi
uliendelea vizuri huku wapiga kura wakionekana kuwa watulivu.
Msimamizi wa uchaguzi msaidizi,Rose
Masondole alisema kuwapo wapiga kura bado mpaka mchana walikuwa wamepokea kesi
tisa.
Katika kituo cha Mbuyuni, alisema wagombea
wa nafasi ya mwenyekiti walifika kituo hapo wakiwa na madaftari ya wapigakura
Msimamizi wa uchaguzi kwenye kituo hicho,Ibrahim
Mabewa alisema kitendo hicho
kilisababisha mvurugano mkubwa.
Katika kituo cha Kinondoni Mjini, wananchi
walilazimika kupigia kura katika eneo la Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT).
Hali hiyo, ilitokana na kituo chao cha
awali kuhamishwa baada ya kutokea vurugu zilizo daiwa kusababishwa na mgombea wa
nafasi ya uenyekiti wa CCM.
MWANZA
Taarifa kutoka mkoani Mwanza, zinasema uchaguzi
wa Mtaa wa Ibungilo ‘B’ Kata ya Nyamanoro uliotarajiwa kufanyika jana
ulikumbwa na miujiza.
Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela,
Justine Lukaza na Ofisa Mtendaji wa kata ya Nyamanoro wakiwa na askari polisi
walibandika matokeo ya uchaguzi uliofanyika Desemba 14, mwaka huu.
Matokeo hayo yanaonyesha mgombea wa CCM,
Christopher Mugeta kuwa mshindi kwa kupata kura 448 dhidi ya Ramadhan Said wa Chadema
ambaye alipata kura 321 kati ya kura 769
zilizopigwa.
Kutokana na hatua hiyo, Mbunge wa Ilemela,
Highness Kiwia (Chadema) naye amemsimika Said kuwa ndiye mwenyekiti wa mtaa huo
akipinga matokeo hayo kwa vile walikubaliana uchaguzi kurudiwa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana,
Kiwia alisema wameamua kumsimika Said baada ya viongozi wa kata ya Nyamanoro na
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kukiuka makubaliano waliyofikia wiki
iliyopta.
“Mara
nyingi tunapopigania haki zetu tumekuwa tukionekana watu wenye vurugu, angalia
kitendo cha kubandika matokeo ya Desemba 14, mwaka huu ambayo yalivurugika
baada ya kura kuzidi na kumlazimu mtendaji wa kata kuahirisha uchaguzi huo hadi
Desemba 21, mwaka huu..kitendo hiki kinaonyesha utumiaji wa nguvu, tutakipinga
kwa nguvu zote,” alisema.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Lukaza alikanusha kuwapo kwa dosari katika
uchaguzi wa Desemba 14.
Alisema matokeo ya uchaguzi huo yaliahirishwa
kutangazwa kutokana na wafuasi wa CCM kufanyiwa vurugu.
Comments
Post a Comment