MISA TAN, MBATIA AKIWA VUNJO NA WALIMU
Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa
Afrika(MISATAN) Bwana Andrew Marawiti akizungumza jambo wakati akifungua
kongamano na maafisa habari wa taasisi za serikali zilizofanyika jana jijini
Dar es Salaam.
Na Mwandishi wetu
Maafisa habari mbalimbali
kutoka wizara na mihimili tofauti ya nchi, jana walikutana katika hoteli ya JB
Belmont hapa Dar es Salaam kujadili changamoto wanazo kumbana nazo wakati kwa
kutoa taarifa kwa wananchi.
Kongamano hilo linafuatia
matokeo ya utafiti wa upatikanaji taarifa kwenye taasisi za umma uliofanywa na
Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA) nakuzinduliwa rasmi siku
ya tarehe 28 Septemba, ambayo pia ni Siku ya Kimataifa ya Haki ya Kupata
Taarifa.
Miongoni mwa taasisi
zilizoshiriki katika kongamano hilo ni Bunge, Mahakama, Wizara ya Katiba na
Sheria, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Wizara ya Nishati na Madini,
Idara ya Habari Maelezo, Mamlaka ya Taifa ya Vitambulisho (NIDA) na Idara ya
Taifa ya Takwimu. Wizara za Afya na Mambo ya Nje hazikuweza kuwakilishwa licha
ya kupata mwaliko.
Mwanasheria kutoka Taasisi Kitaifa ya Msaada wa Kisheria (National
Organization of Legal Assistance-nola) Bwana James Malenga akisisitiza
jambo alipokuwa anawasilisha mada yake kwenye kongamano hilo la maafisa habari
wa taasisi za kiserikali lililoandaliwa na Misa-Tanzania.
Afisa Habari na Utafiti wa Misa-TanzaniaBwana Sengiyumva
Gasirigwa akitoa ufafanuzi kwenye mada aliyokuwa anaiwasilisha kwenye
kongamano la maafisa habari wa taasisi za kiserikali(hawapo picha)
Mfanyakazi wa Misa-TanzaniaBwana Idrisa Abdallah akizungumzia adha
anazozipata anapokuwa anakwenda taasisi na idara mbalimbali za serikali
kupeleka barua ama maombi ya taarifa.
Afisa habari wa Mahakama Bi. Mary C. Gwera akizungumza jinsi ofisi
yake ilivyopokea Tuzo ya Kufuli na ambavyo imekuwa chachu ya mabadiliko katika
kutoa taarifa kwa umma.
Afisa Mwandamizi wa habari kutoka Idara ya Habari Maelezo Bwana Abraham
Nyantori akielezea changamoto za utoaji taarifa katika taasisi na idara za
serikali.
Maafisa habari wakifuatilia kwa umakini mada ya Umuhimu wa Kutoa/Kupata
Taarifa serikalini kutoka kwa mwanasheria wa kujitegemea Bwana James Marenga.
Kaimu Mkurugenzi wa Misa-Tanzania
Bwana Andrew Marawiti akitoa shukrani wa wageni waliofika kwenye
kongamano hilo.
CWT WAADHIMISHA SIKU YA WALIMU DUNIANI
Mratibu
wa Uhakiki wa Ubora wa Elimu kutoka Shirika la Kijamii la Masuala ya Elimu (Haki
Elimu), Robert Mihayo akitoa mada kuhusu Ubora wa Elimu Tanzania wakati wa semina
ya maadhimisho ya Siku ya Walimu Duniani iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Semina hiyo iliandaliwa na TENMET kwa kushirikiana na Chama Cha Walimu Tanzania
(CWT).
Mratibu
wa Uhakiki wa Ubora wa Elimu kutoka Shirika la Kijamii la Masuala ya Elimu (Haki
Elimu), Robert Mihayo akitoa mada kuhusu Ubora wa Elimu Tanzania wakati wa semina
ya maadhimisho ya Siku ya Walimu Duniani iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Semina hiyo iliandaliwa na TEN/MET kwa kushirikiana na Chama Cha Walimu Tanzania
(CWT).
Ofisa
Mradi wa TEN/MET, Alistidia Kamugisha (kulia), Meneja wa Fedha na
Utawala (TEN/MET), Beatrice Malya (katikati) na Mratibu wa TEN/MET,
Cathleene Sekwao.
Baadhi ya washiriki wa semina hiyo.
Baadhi ya washiriki wa semina hiyo.
Neema Kitundu kutoka National Coordinator Fawetz.
Neema Kitundu kutoka National Coordinator Fawetz.
Mkurugenzi
Msaidizi Idara ya Ukaguzi wa Shule Wizara ya Elimu ya Ufundi ya Ufundi,
Dk. Edicome Cornel Shirima akitoa mada katika semina hiyo.
Mkurugenzi Mafunzo ya Ualimu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Bakari Issa akitoa mada katika semina hiyo.
Peter Mlimahadala kutoka Chama cha Walimu Tanzania akichangia mada katika semina hiyo.
Mratibu wa TEN/MET, Anthony Mwakibinga.
Mkurugenzi Mafunzo ya Ualimu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Bakari Issa akitoa mada katika semina hiyo.
Peter Mlimahadala kutoka Chama cha Walimu Tanzania akichangia mada katika semina hiyo.
Mratibu wa TEN/MET, Anthony Mwakibinga.
MBUNGE JAMES MBATIA ATEMBELEA MAKABURI YA WAZAZI WAKE NYUMBANI KWAO KILUA VUNJO
Marehemu ,Mwalimu Francis.W,Mbatia,Baba mzazi wa Mbunge wa Kuteuliwa James Mbatia. |
Marehemu ,Philomena Francis Mbatia,Mama mzazi wa Mbunge wa Kuteuliwa James Mbatia. |
Makaburi ya wazazi wa Mbunge wa kuteuliwa James Mbatia yaliyoko nyumbani kwao kata ya Vunjo Mangaribi-Kilua Vunjo wilaya ya Moshi vijijini. |
Mh James Mbatia akiwa na viongozi wa Chama cha NCCR-Mageuzi mkoa wa Kilimanjaro wakati alipotembelea eneo hilo. |
Mh James Mbatia akifanya sala mbele ya Makaburi ya Wazazi wake alipotembelea nyumbani kwao. |
Mh James Mbatia akiwasilimulia viongozi alioambata nao mambo mbalimbali ambayo wazazi wake walipenda kumwelekeza yakiwemo maneno ambaye baadae aliamua yaandikwe juu ya makaburi hayo. |
Mh Mbatia akiondoka katika eneo la Makaburi ya wazazi wake.Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya kaskazini. |
KAMPUNI YA COMSOFT YA UJERUMANI YA WAPIGA MSASA WAHANDISI NA WATAALAMU WA MASUALA YA USAFIRI WA ANGA BARANI AFRIKA.
Kaimu Mkutugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)
Charles Chacha (katikati) na Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya
COMSOFT Mr.Manfred Schmid (kushoto)wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi
wa Mradi wa Comsoft Dr.Gunther Hellstrn ( kulia )wakati alipokuwa
akitoa mada juu ya usimamizi wa mitambo ya ADS-B ambayo inatumika kwa
ajilia ya usalama wa Anga wakati semina iliyowahusisha wahandisi wa
mamlaka ya usafiri wa Anga Barani Afrika iliofanyika leo ktika Hoteli ya
Serena jijini Dar es Salaam ikiwa imeandaliwa na COMSOFT ya Ujeremani.
Baadhi
ya Wahandisi na wataalamu wa masuala ya usafiri wa anga kutoka barani
Afrika wakimsikilza kwa makini Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya
COMSOFT Mr.Manfred Schmid (kushoto) wakati wa semina ya usimamizi wa
mitambo ya ADS-B ambayo inatumika kwa ajilia ya usalama wa ndege ikiwa
kwenye anga husika.iliyofanyika katika hoteli ya serene leo jijini Dar
es Salaam.
Mkurugenzi
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya COMSOFT Mr.Manfred Schmid na Mkurugenzi
wa Mradi wa Comsoft Dr.Gunther Hellstrn ( kulia ) wakimsikilza kwa
makini mtaaramu wa kuongoza ndege kutoka Uganda (UGATCA) Magret Kagendo
wakati alipokuwa akiuliza swali wakati wa semina iliyowashirikisha
wahandisi na wataalamu wa Mamlaka ya usafiri wa Anga barani Afrika
iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi
ya Wahandisi na wataalamu wa masuala ya usafiri wa anga kutoka barani
Afrika wakimsikilza Mkurugenzi wa Mradi wa Comsoft Dr.Gunther Hellstrn (
kulia ) juu ya masuala ya usimamizi wa usalama wa Anga katika semina
iliofanyika leo katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam
Kaimu
Mkutugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Charles
Chacha (katikati) na Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya COMSOFT
Mr.Manfred Schmid (kulia)wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Mradi
wa Comsoft Dr.Gunther Hellstrn ( kulia )wakati alipokuwa akiongelea
masuala ya usimamizi wa usalama wa Anga katika semina iliyowahusisha
wahandisi wa mamlaka ya usafiri wa Anga Barani Afrika uliofanyika leo
ktika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Kaimu
Mkutugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Charles
Chacha (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya COMSOFT
Mr.Manfred Schmid (kulia)wakiwa miongoni mwa washiriki wa semina ya
wahandisi na wataalamu wa uendeshaji wa mamlaka ya usafiri wa Anga
barani Afrika iliyofanyika leo katika hoteli ya Serena,jijini Dar es
Salaam,Semina hiyo imeandaliwa na kampuni ya Comsoft ya Ujerumani ambao
ni wataalamu wa mitambo inayotumika kwa ajili ya usalama ndege wakati
ikiwa anga husika.
Washiriki
wa semina yamasuala ya mitambo ya ADS-B amabayo inatumika kwa ajili ya
usalama wa Anga na Uangalizi wa Ndege inapotoka kwenye anga husika na
kwenda naga nyingine iliyo wahusisha Wahandisi na wataaramu wa masuala
ya usafiri wa anga kutoka barani Afrika ,wakifuatilia moja ya mada
zilizokuwa zikitolewa kwenye semina hiyo iliyoandaliwa na COMSOFT
jijini Dar es Salaam.
Comments
Post a Comment