DAWASA NA HABITAT WALETA MAPINDUZI KATIKA ELIMU DAR


Meneja wa Mradi wa ujenzi wa mtambo wa nishati endelevu inayohifadhi mazingira (Biogas) kutoka UN-HABITAT Phillemon Mutashubirwa akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari walipotembelea mradi huo unaotekelezwa katika shule ya sekondari Manzese mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam.


Meneja Uhusiano wa Jamii Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es salaam (DAWASA) Bi. Neli Msuya alipokuwa akiongea na waandishi wa habari mwishoni mwa wiki walipotembelea mradi wa ujenzi wa mtambo wa nishati endelevu inayohifadhi mazingira (Biogas) katika shule ya sekondari Manzese iliyopo Mtaa wa Chakula bora kata ya Manzese Wilaya Kinondoni jijini Dar es salaam. Mradi huo unatekelezwa shuleni hapo na DAWASA kwa kushirikiana na Shirika la Mpango wa Makazi la Umoja wa Mataifa (UN-HABITAT).
 




Mratibu wa Mradi ujenzi wa  mtambo wa kuzalisha gesi ambayo ni nishati endelevu inayohifadhi mazingira (Biogas) kutoka Taasisi ya Kuendeleza Nishati Asilia na Uhifadhi wa Mazingira (TaTEDO)  Shima Sago akieleza faida zitokanazo na biogas kwa waandishi wa habari walipotembelea mradi huo unaotekelezwa katika shule ya sekondari Manzese mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam.
 


Mwalimu wa Taaluma wa shule ya sekondari Manzese Zubeda Kindamba akiushukuru uongozi wa DAWASA kwa kuendelea kuiunga mkono shule yao katika masuala mbalimbali ukiwemo Mradi wa ujenzi wa  mtambo wa kuzalisha gesi asilia shuleni hapo.

 Mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya sekondari Manzese anayesoma masomo ya mchepuo wa sayansi Noela Shirima akielezea kwa waandishi wa habari namna watakavyonufaika mara utakapokamikika mradi wa gesi asilia itakayozalishwa na amesema kuwa kujengwa mradi wa gesi na maabara utawasaidia shuleni hapo kwa manufaa ya kupata elimu bora.

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Chakula bora Kata ya Manzes Salehe Rashidi akielezea kwa waandishi wa habari walipotembelea shule ya sekondari Manzese mwishoni mwa wiki namna wananchi wake wanavyoshikiana na Uongozi wa shule hiyo katika kujali taaluma ya wanafunzi na afya zao kwa kufanya usafi katika maeneo yanayozunguka shule.
Mutashubirwa na Nelly, wakienda kukagua shimo linalochimbwa kuhusu kutebgebeza gesi

 
 Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari Manzese wakishiriki kuandaa eneo utakapojengwa mtambo wa kuzailsha gesi shuleni hapo.

Mafundi wa Tatedo, wakiendelea na ujenzi
 Darasa la Maabara
 Majirani na shule  hiyo wakitawanya mchanga uliotokana na uchumbwajai wa shimo lililosababisha kuzibwa kwa barabara ya mtaa huo

Comments

Popular posts from this blog

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

AMANI YETU TUILINDE NAIBU WAZIRI CHANDE AZUNGUMZA KATIKA IJITIMAI JIJINI DODOMA

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.