PPF NA SHEREHE ZA MWAKA WAO DAR
Kaimu
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Dr Aggrey
Mlimuka akizungumza na wafanyakazi wa mfuko wa pensheni wa PPF wakati wa
sherehe ya Mwaka iliyofanyika katika Ukumbi wa Blue Pearl Ubungo Jijini
Dar Es Salaam Mwishoni mwa wiki.
Kaimu
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Dr Aggrey
Mlimuka akiwapongeza Vijana wanaounda kundi la The Voice ambao ni
wasanii wa fani ya Akapela mara baada ya Kutoa burudani katika sherehe
ya Mwaka ya Mfuko wa Pensheni wa PPF iliyofanyika mwishoni mwa wiki
katika Hoteli ya Blue Pearl iliyopo Ubungo Jijini Dar Es Salaam.
Kundi
la The Voice likitoa burudani katika sherehe ya Mwaka ya Mfuko wa
Pensheni wa PPF iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika Hoteli ya Blue
Pearl.
Baadhi
ya wafanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF wakifuatilia matukio
yaliyokuwa yakiendelea katika Sherehe ya Mwaka ya Wafanyakazi wa Mfuko
wa Pensheni wa PPF iliyofanyika mwishoni mwa Wiki katika Ukumbi wa Blue
Pearl.
Afisa
Mahusiano wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bi Janeth Ezekiel akipokea cheti
na zawadi kutoka Kwa Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Udhamini wa Mfuko wa
Pensheni wa PPF, Dr Aggrey Mlimuka mara baada ya kutangazwa kuwa
mfanyakazi bora wa mwaka 2013 kutoka Idara ya Mahusiano na Masoko ya
Mfuko wa Pensheni wa PPF katika sherehe ya mwaka ya PPF iliyofanyika
mwishoni mwa wiki katika Hoteli ya Blue Pearl, Jijini Dar Es Salaam
Pichani
Juu Ni baadhi ya wafanyakazi kutoka Idara Mbalimbali za Mfuko wa
Pensheni wa PPF waliojipatia zawadi kwa kuwa wafanyakazi bora wa Mwaka
2013.
Wafanyakazi
wa PPF wakifuatilia Burudani iliyokuwa ikitolewa na Kundi la The Voice
katika Sherehe ya Mwaka ya PPF iliyofanyika mwishoni mwa Wiki katika
Hotel ya Blue Pearl.
Mmoja
wa wafanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF akimtunza Mmoja ya waimbaji
wa kundi la the voice lililokuwa likitoa burudani wakati wa sherehe ya
Mwaka ya Mfuko wa Pensheni wa PPF iliyofanyika Mwisho mwa Wiki katika
hoteli ya Blue Pearl, Jijini Dar
Wadau
wakiserebuka Muziki mara baada ya wafanyakazi bora kupewa motisha na
zawadi zao katika sherehe ya Mwaka ya PPF iliyofanyika Mwishoni mwa Wiki
katika Hoteli ya Blue Pearl, Ubungo Jijini Dar Es Salaam.
KINANA ASISITIZA WANANCHI BAGAMOYO KUJIUNGA NA MIFUKO YA AFYA YA JAMII
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na
Uenezi Nape Nnauye wakiwapungia mkono wakazi wa Bagamoyo wakati
wakiwasili kwenye uwanja wa mkutano wa shule ya Msingi Jitegemee.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimpa mkono wa pongezi mshahiri
maarufu wa CCM mkoa wa Pwani Ndugu Ali Pongwe baada ya kutoa ushairi
mzuri kabla ya kuanza kwa mkutano.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kata ya
Magomeni wilaya ya Bagamoyo ambapo aliwasisitiza kujiunga na mfuko wa
afya ya jamii pamoja na wazazi kuwapeleka watoto shule pia aliwashauri
wazazi kuchagua watu wenye shughuli zao kuingia kwenye kamati za shule
kwani kutasaidia sana kupunguza michango isiyo ya lazima.
Wananchi wa kata ya Magomeni wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
Mkuu
wa Mkoa wa Pwani Mheshimiwa Mwantumu Mahiza akihutubia wakazi wa kata ya
Magomeni na kuwataka kuhakikisha watoto watakaochaguliwa kuingia
sekondari wanaenda shule kwani kushindwa kufanya hivyo ni kurudisha
nyuma maendeleo.Pia aliwataka wananchi wachunge afya zao kwani elimu ya
maambukizi ya ukimwi inatolewa ya kutosha hivyo kila mtu anapaswa kuwa
makini na afya yake.
Sehemu ya watu waliohudhuria mkutano.
Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa kata ya
Magomeni ambapo alitoa sifa kwa Mkuu wa mkoa wa Pwani kwa utendaji wake
wenye ufanisi mkubwa pia aliwaambia wananchi hao kuwa vyama vya siasa
ndio vimeshafika muda wake kwani havina sera na vimeshindwa kuja na sera
mbadala ya kuleta maendeleo ya kiuchumi nchini.
Wananchi
wakimsikiliza Nape Nnauye ambaye pia aliwataka watendaji wa Serikali
kuwa karibu na wananchi kwani kutasaidia kufanikisha maendeleo na
kuondoa sintofahamu za wananchi wanaotaka kujua taarifa za maendeleo ya
miradi au maeneo husika.
Mbunge
wa Jimbo la Bagamoyo Dk.Shukuru Kawambwa akihutubia wakazi wa jimbo
lake wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya shule
ya msingi Jitegemee ambapo aliwaambia kero za michango midogo midogo
zinaondolewa .
Katibu
wa CCM mkoa wa Pwani Joyce Masunga akihutubia wakazi wa kata ya
Magomeni ambapo aliwaambia wanawake kutokuwa nyuma katika kuomba nafasi
za uongozi katika chaguzi zinazokuja.
Mmoja wa wananchi waliofika kwenye mkutano akiuliza swali kwa Katibu Mkuu wa CCM wakati wa mkutano .
Diwani wa kata ya Magomeni .Mwanaharusi Jarufu akijibu moja ya maswali yaliotoka kwa wananchi.
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo akijibu maswali kutoka kwa wananchi
Sehemu
ya wanachama wapya waliopokea kadi zao za uanachama leo mbele ya Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ambapo zaidi ya wanachama 338
walijiunga na CCM.
UMOJA WA MATAIFA WATAKA CHANZO CHA SIASA KALI ZINAZOLETEA MIGOGORO KICHUNGUZWE
Mgeni
rasmi kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya Amani, Waziri wa Afya
na Ustawi wa Jamii, Mh. Seif Rashid akiwasili kwenye viwanja vya Mnazi
Mmoja kuhudhuria maadhimisho hayo na kupokelewa na Makamu Mwenyekiti wa
Chama cha Albino Tanzania (TAS), Joseph Masasi (wa pili kulia), Kamishna
wa Ustawi wa Jamii, Bw. Dunford Makala (katikati) na Kamishna wa Tume
ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Tanzania , Bw. Ali Rajab (kulia)
pamoja na viongozi wengine taasisi ya watu wenye ulemavu wa ngozi
(Albinizim)
Na Mwandishi wetu
WAKATI
Katibu Mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki-moon anahimiza serikali duniani
kutafuta chanzo cha kukosekana kwa amani na kuongezeka kwa watu wenye
misimamo mikali, wasemaji katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa amani
Duniani wameitaka serikali ya Tanzania kutupia macho makali mauaji ya
albino nchini.
Akimwakilisha
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa katika adhimisho lililofanyika viwanja
vya Mnazi mmoja leo Mratibu mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi
mkazi wa UNDP nchini Alvaro Rodriguez, alisema ili kudumisha amani kuna
mambo mengi yanatakiwa kufanyiwa kazi hasa kutambua chanzo cha migogoro
inayosababisha msuguano mkubwa katika jamii na kukosekana kwa amani.
Alisema
amani ina maana kubwa kwa jamii na ndio maana Umoja wa mataifa miaka 13
iliyopita iliamua kuadhimisha siku hiyo kwa lengo la kushawsihi makundi
yanayosigana kupata nafasi ya kuzungumzia na kuona maana ya amani.
Alisema
pamoja na kuwepo kwa hatua kubwa tangu kupitishwa kwa azimio la Umoja
wa Mataifa la kuadhimisha amani, safari ya kufikia amani ni ndefu na ili
kufanikiwa pande zote ni lazima kwenda hatua kwa hatua kwa
kushirikiana.
Alisema
mafanikio ambayo yamepatikana ni pamoja na UN kufanikiwa kufundisha
kada ya habari juu ya uandishi katika mazingira tete na kusaidia
majadiliano ya kitamaduni yanagusa masuala ya amani.
Mtaalam
wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce
Temu (katikati) akimtambulisha Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa
Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP)
nchini, Alvaro Rodriguez (wa pili kushoto) mara baada ya kuwasili kwa
Katibu Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini
Tanzania (THBUB), Bi. Mary Massay.
Aidha
alisema kwamba wanafanyakazi na Wizara ya mambo ya ndani kuhakikisha
kwamba wanastawisha mipango yote inayolenga kuzuia ghasia na kuboresha
mipango inayoimarisha amani.
Akihutubia
bada ya mashuhuda kuzungumzia hali ya tishio la amani nchini Tanzania
hasa la kukosekana kwa amani miongoni mwa watu wenye ulemavu wa ngozi
albino, Mwakilishi huyo wa Umoja wa Mataifa aliipongeza serikali ya
Tanzania kw ajuhudi zake za kuimarisha amani katika kanda ya maziwa
makuu na kushiriki katika operesheni mbalimbali za Umoja wa Mataifa
ziliziolenga kuleta hali bora zaidi ya maisha kwa watu wanaoishi katika
hekaheka za kivita.
Akiwa
na mwezi mmoja tangu awalisili nchini mwakilishi huyo wa Umoja wa
Mataifa nchini amesema kwamba anatarajia kuendelea kuunga mkono juhudi
za serikali na wananchi wa Tanzania kuhakikisha taifa la Tanzania
linaendelea kuwa na amanai.
Wakati
Mwakilishi huyo amesema kwamba watu wengi duniani wanawaonea gere
wananchi wa Tanzania kwa amani wlaiyonayo, mwakilishi wa Under the Same
Sun, Vicky Ntetema ametaka kupitiwa upya kwa sheria ya uchawi ya mwaka
1928 iliyofanyiwa mabadiliko mwaka 2002 ili kukabiliana na mauaji ya
albino nchini ambayo kwa kiasi kikubwa yanachochewa na waganga wa
kienyeji.
Mratibu
Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez
akisalimiana na Mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya
Amani, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Seif Rashid meza kuu.
Alisema
sheria hiyo ina mwanya mkubwa wa wauaji kucheza nayo na kusababisha
sehemu kubwa ya kesi zilizopo kushindwa kuwatia hatiani wahusika.
Alisema wakati tukielekea katika uchaguzi mkuu mauaji ya albino na ukataji wa viungo umeongezeka.
Tanzania
ikiwa ni miongoni mwa nchi 25 za afrika zinazofanya ukatili dhidi ya
walemavu wa ngozi, toka mwaka 2006 watu 74 wameuawa, 56 wamenusurika na
11 wameongezewa ulemavu huku makaburi 18 ya albino yakinajisiwa kwa
kufukuliwa.
Watu
wa kituo cha haki za binadamu wamesema pamoja na kuwepo na matukio 120
ya ukatili dhidi ya albino kesi 11 tu ndio zilizofikishwa mahakamani
huku tano zikiwa zimekatiwa hukumu ambazo hazijaridhisha.
Vicky
alisema katika matukio yote hayo chanzo ni ushirikina lakini kutokana
na kukosekana zimeshindikana kuzimaliza zinavyotakiwa.
Brass
band ya jeshi la Magereza ikiongoza maandamano ya kuadhimisha siku ya
kimataifa ya amani wakiwasili kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar
es Salaam wakati wa maadhimisho hayo jana.
Vicky
aliitaka jamii kuwalinda albino kwani serikali pekee haiwezi kufanya
kitu chochote huku akisema kwamba hesabu ya albino mmoja katika kila
wananchi 1,400 haiwezi kulindwa kwa dhati na serikali kutokana na
idadi ya polisi kutokua sawa na wananchi.
Aidha
alishauri serikali kutoa msaada wa kisheria kwa waathirika kabla ya
kuingia mahakamani ili waweze kusimulia vyema kadhia zao na pia
wasiangushwe na wanasheria ambao wanatumia udhaifu wa kisheria kuwatoa
watuhumiwa hatiani.
Pamoja
na Vicky Ntetema kushawishi wananchi kulinda albino na kuwafichua
wauaji Kaimu Mufti Sheikh Ismail Habibu Makusanya ameitaka serikali
kuhakikisha kwamba kila mwananchi anapata utulivu wa kutosha kuendelea
na shughuli zaka na kuhimiza mahakama kutenda haki.
Aliwakumbusha
wananchi kama alivyosema Sydina Omar kwamba kila mmoja ataulizwa
amefanya nini kukomesha madhila katika jamii wakati wa kiama na kusema
serikali isipowajibika itasema nini na wananchi nao pia watajibu nini.
Pichani
ni baadhi wadau kutoka taasisi mbalimbali pamoja na watu wenye ulemavu
wa ngozi (Albinism) wakiwasili kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja huku
wakiwa wamebeba mabango yenye jumbe mbalimbali za kuhamasisha amani
nchini na kupinga mauji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) nchini
wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya amani iliyofanyika jana
jijini Dar.
Alisema
amani hailetwi kama mvua , inatafutwa na kusema watu wasipotafuta amani
na kuhakikisha amani inakuwapo itakuwa shida kubwa kwa taifa hili
ambalo miaka yote limeogelea katika bahari ya amani.
Aliwasihi waumini wa Kiislamu na wananchi wengine kuhakukisha kwamba amani inakuwa ajenda ya kudumu kila wanapokutana pamoja.
Katika
maadhimisha hayo ambapo wananchi walianza maandamano shule ya Uhuru
Mchanganyiko hadi viwanja vya Mnazi mmoja, mgeni rasmi Waziri wa Afya na
Ustawi wa jamii Dk Seif Rashid alisema serikali imejipanga kuhakikisha
inakomesha mauaji ya albino na kuwataka wananchi kuisaidia kwa kutokuwa
waoga kutoa ushahidi na pia kuwaripoti watuhumiwa.
Alisema
kauli mbiu ya mwaka huu ya haki ya amani kwa watu wote, komesha mauaji
ya albino inahamasiaha umma wa Tanzania kulaani,kukemea na kukomesha
mauaji kwani yanakwenda kinyume na katiba ya Tanzania ya mwaka 1977
ibara ya 14 ambayo inaeleza kwamba kila mtu ana haki ya kupata hifadhi
katika jamii.
Aidha
waziri alitaka kutekelezwa kwa agizo lake kuhusu tiba mbadala na za
asili na kusema serikali itaendelea kulinda amani na kutoa ulinzi kwa
wathirika.
Meza kuu ikipoeka maandamano ya siku ya kimataifa ya amani kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Makamu
Mwenyekiti wa Chama cha Albino Tanzania (TAS), Joseph Masasi akitoa
neno la ukaribisho kwa mgeni rasmi Mh. Seif Rashid (wa pili kulia).
Kutoka kushoto ni Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na
mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini,
Alvaro Rodriguez, Kamishna wa Ustawi wa Jamii, Bw. Dunford Makala,
Balozi wa Uturuki nchini, Mh. Ali Davutoglu.
Mgeni
rasmi kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya Amani, Waziri wa Afya
na Ustawi wa Jamii, Mh. Seif Rashid, akisoma hotuba kwenye maadhimisho
ya siku ya kimataifa ya amani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi
Mmoja jijini Dar es Salaam.
Mratibu
Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, akisoma
ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki-Moon kwenye
maadhimisho ya siku ya kimataifa ya amani duniani.
Mratibu
Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez
akipongezwa na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mh. Ali Davutoglu
baada ya kusoma ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
Mkurugenzi
Mtendaji wa shirika la UNDER THE SAME SUN, Vicky Ntetema akisoma risala
yake kwa mgeni rasmi wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya
amani iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Kaimu
Mufti Sheikh Ismail Habibu Makusanya, akizungumza kwenye maadhimisho
hayo ambapo alilaani vikali mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi
(Albinizim) na kusema kuwa watu wote wanaoshiriki katika mauaji hayo
kamwe hawatoiona Pepo ya Mwenyezi Mungu.
Balozi
wa Uturuki nchini Tanzania, Mh. Ali Davutoglu akisoma ujumbe kwa niaba
wa umoja wa mabalozi kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya amani
duniani.
Baadhi ya wadau kutoka taasisi na asasi mbalimbali nchini walioshiriki kwenye maadhimisho hayo.
Katibu
Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini Tanzania
(THBUB), Mary Massay akitoa nasaha kutoka kwa Tume hiyo, ambapo
alitoa rai kwa mtu yeyote yule ambaye ana malalamiko au matatizo katika
Haki za Binadamu anakaribishwa kwenye tume hiyo kwa ajili kupata msaada
wa kisheria.
Shuhuda
aliyenusurika kwenye mauaji ya Albino ambaye amekatwa mikono yote
miwili, Mariam Stanford akitoa ushuhuda wake na killio chake mbele ya
meza na wageni waalikwa waliohudhuria sherehe za maadhimisho ya siku ya
kimataifa ya amani iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam kwenye viwanja
vya Mnazi mmoja.
Mke
wa Balozi wa Uturuki nchini Yesim Davutoglu, akilia kwa uchungu baada
ya kusikia shuhuda kutoka kwa mhanga wa mauaji ya Albino aliyekatwa
mikono yote miwili, Mariam Stanford (hayupo pichani) ambaye hadi sasa
anapewa matunzo na Shirika la Under The Same Sun.
Mkurugenzi
Mtendaji wa shirika la UNDER THE SAME SUN, Vicky Ntetema akimfariji mke
wa Balozi wa Uturuki nchini Yesim Davutoglu, wakati wa maadhimisho ya
siku ya kimataifa ya amani duniani iliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi
mmoja jijini Dar.
MKUU WA WILAYA YA MAKETE AFANYA KIKAO CHA MAENDELEO NA WANAMAKETE WAISHIO JIJINI DAR
Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro akizungumza katika kikao hicho.
Wananchi
waliozaliwa wilayani Makete mkoani Njombe ambao wanaishi nje ya wilaya
hiyo, wameshauriwa kuipenda wilaya yao kwa kuja kuwekeza pamoja na
kushiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo ndani ya wilaya hiyo
Rai
hiyo imetolewa hii leo na Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro
katika kikao baina yake na wananchi wa Makete waishio jijini Dar es
Salaam kilichofanyika jijini humo
Katika
kikao hicho mkuu wa wilaya amewashirikisha mambo mengi ya kimaendeleo
katika wilaya ya Makete ikiwemo uwepo wa shule ya sekondari ya wasichana
ya Makete Girls secondary ambayo pamoja na kuanza kufanya kazi bado
inakabiliwa na changamoto mbalimbali
Mh.
Matiro amezitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na ukosefu wa bweni na
kuwa wanafunzi wanalala kwenye vyumba vilivyojengwa kwa ajili ya
madarasa, bwalo, jiko pamoja na maabara ambavyo vinatakiwa viwepo
Amewaomba
wananchi hao kuunga mkono kwa jinsi Mungu alivyowajalia na kwamba
yeyote atakayejisikia kuchangia anaombwa kufanya hivyo kwani kila mmoja
kwa nafasi yake ana mchango katika shule hiyo ili iondokane na
changamoto hizo
"Ndugu
zangu wilaya yetu inawatambua sana. tunaomba na tunahitaji sana
ushirikiano wenu katika maendeleo ya makete, tukishirikiana kwa pamoja
kwa kadri Mungu alivyotujalia kwa hakika shule hii itaimarika sana"
amesema Matiro
Kwa
upande wao washiriki wameoneshwa kufurahishwa na maendeleo ya kasi
katika wilaya ya makete huku wakiipogeza serikali kwa juhudi zake za
maendeleo hasa katika elimu, barabara, umeme pamoja na mambo mengine
huku wakisema wataunga mkono maendeleo ya wilaya yao kwa kadri ya uwezo
wao
Pia
wameonesha kufurahishwa na Matiro kuwatafuta na kuzungumza nao kwani
wamesema amekuwa mkuu wa wilaya wa kwanza kuzungumza nao toka wilaya
hiyo imeanzishwa na kumtaka kuwa na moyo wa kuipenda wilaya ya Makete
kama mkuu wa wilaya
Wakiwa katika picha ya pamoja na mkuu wa wilaya.
Baada ya kushirikishwa hivyo wameahidi kushirikiana na mkuu huyo wa wilaya kutatua changamoto hizo
RASIMU YA KATIBA MPYA ILIYOPENDEKEZWA KUWASILISHWA BUNGENI SEPTEMBA 24 MWAKA HUU
Na Benedict Liwenga na Magreth Kinabo.
RASIMU ya Katiba Mpya iliyopendekezwa inatarajiwa kuwasilishwa katika Bunge Maalum la Katiba Septemba 24, mwaka huu.
RASIMU ya Katiba Mpya iliyopendekezwa inatarajiwa kuwasilishwa katika Bunge Maalum la Katiba Septemba 24, mwaka huu.
Mabadiliko
hayo yametangazwa leo jioni na Katibu wa Bunge Maalum la Katiba, Yahya
Khamis Hamad wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini
kwake.
Aidha
Katibu huyo amesema uamuzi wa mabadiliko hayo, umetokana na kufanyika
kikao baina ya Kamati ya Uongozi wa Bunge hilo na Mwenyekiti wa Kamati
ya Uandishi.
Hata
hivyo Katibu huyo amesema kuwa kazi ya uandishi wa Rasimu hiyo
imeshakamilika na kazi iliyobakia ni kuipitia kwa makini, hali
iliyosababisha mabadiliko ya uwasilishaji wa Rasimu hiyo katika Bunge
hilo, uliopangwa kufanyika hapo kesho Septemba 22, mwaka huu.
“Uwasilishwaji
wa Rasimu ya Katiba inayopendekezwa sasa utafanywa siku ya Septemba 24,
mwaka huu, ” alisema Katibu wa Bunge hilo.
“Kamati
ya uongozi imeona kuwa ni busara na kupewa siku mbili kwa ajili ya
kuipitia upya ile kazi ambayo wameifanya ili kufikia tarehe 24 kutoa
kitu makini, napenda niwahakikishie wananchi kuwa kitu kizuri kinakuja.
Aliongeza
kuwa Kamati ya Uongozi ya Bunge hilo, inatarajia kukabidhiwa Rasimu ya
Katiba Mpya iliyopendekezwa tarehe 23 Septemba, mwaka huu kutoka kwa
Kamati ya Uandishi wa Bunge hilo.
Aidha,
Katibu huyo ameeleza sababu ya uairishwaji wa uwasilishwaji wa Rasimu
hiyo Bungeni hapo kutokana na ugumu, umakini na uzito wa kazi yenyewe.
“Tulikuwa
tumepanga hapo tokea awali kufanya kikao na Kamati ya Uongozi asubuhi
tukafanya mchana na hata jioni kila wakati Kamati ya Uandishi ikawa bado
haijamaliza hiyo kazi na tulivyofanya kikao cha Kamati ya Uongozi hii
jioni tukamuita Mwenyekiti wa Kamati ya uandishi akaonyesha kwamba hiyo
kazi walikuwa wakiifanya usiku na mchana na hadi sasa wamesema
wamemaliza kuandika.
“Lakini
kutokana na namna walivyokuwa wakiifanya hiyo kazi kwa uharaka na
ingawa walikuwa wakiifanya kwa umakini lakini wanahitaji muda wa kuanza
kuipitia kwa makini zaidi kuanzia mwanzo mpaka mwisho hivyo wakaomba
wapewe muda wa siku mbili ya kesho na keshokutwa ili kuweza kuipitia
kazi hiyo kwa umakini,”alisema.
Katibu
wa Bunge hilo, aliongeza kwamba mabadiliko hayo hayataweza kuathiri
upigaji kura uliopangwa kufanyika Septemba 29 hadi 2 Oktoba mwaka huu.
“Tumeacha
siku ya Septemba 29, mwaka huu ili iwe siku ya kuanza kupiga kura na
tumalize 2 Oktoba, mwaka huu ili tuhakikishe kwamba Oktoba 4 , mwaka
tumemaliza hili zoezi,” alisisitiza.
Aidha Katibu huyo alifafanua kuwa ratiba kuhusiana na masuala hayo ataitoa
SIMBA NA WAGOSI WA KAYA TAIFA
Beki wa Simba, Mohamed Hussein (kulia) akichuana na Seleman Rajab. Timu hizo zilitoka sare ya 2-2.
Emmanuel Okwi akiwania mpira na beki wa Coast Union.
Umati wa mashabiki waliofika uwanja wa Taifa.
Mshambuliaji wa Simba, Ramadhan Singano 'Messi' akimiliki mpira huku akizongwa na beki wa Coast Union, Abdallah Mfuko.
Mshambuliaji wa Simba, Haruna Chanongo akiruka daruga la beki wa Coast Union.
Hamis Tambwe akitafuta mbinu za kumtoka beki wa Coast Union.
Hatari katika lango la Coast Union.
Emmanuel Okwi akimtoka beki wa Coast Union.
Kikosi cha Simba.
Kikosi cha Coast Union.
Golikipa wa Coast Union ya Tanga, Shaban Kado akiokoa moja ya hatari langoni mwake.
Wachezaji wa Coast Union wakitoka mapumziko.
Wachezaji wa Simba wakitoka mapumziko.
Benchi la ufundi la Coast Union.
Manahodha wa Simba na Coast Union wakiwa katika picha ya pamoja.
Benchi la ufundi la Simba likiongozwa na Patrick Phil.
Kikundi cha New Mapambano kikitumbuiza wakati Simba ikipambana na Coast Union.
Mashabiki wa Simba wakiwa na uzi wa Simba.
Mashabiki wa Simba wakiishangilia timu yao.
Wachezaji wa Simba wakishangilia bao la kwanza la timu hiyo kabla Coast Union kusawazisha.
Mshambuliaji
wa Simba, Hamis Tambwe akiifungia timu yake bao la pili wakati timu hiyo
ilipopambana na Coast Union ya Tanga katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka
Tanzania Bara uliofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam. Timu hizo zilitoka sare ya 2-2.
Comments
Post a Comment